Karibu
ndugu wasomaji wa wavuti hii, leo napenda kuongelea mambo sita yanayowatia hofu
wanawake kwa waume zao pamoja ustawi wa ndoa zao. Kutokana na tafiti mbalimbali
na uzoefu wa kimazingira kuna hofu nyingi wanazokuwa nazo wanawake dhidi ya
waume zao hasa kwa ndoa changa na ambazo hazikupitia hatua ya uchumba wa muda
mrefu. Kama iliyohada mke na mme hukutana wakiwa wote ni watu wazima
waliyokulia katika mazingira, utamaduni na familia tofauti wakapendana na
kufikia maamuzi ya hiari ya kufunga ndoa. Kutokana na mzingira, makuzi,
utamaduni, mtazamo n.k. watu wanapokuwa wameamua kufunga ndoa hutokea hofu za
kimahusiano za hapa na pale ambazo kila mmoja hujitahidi kuziondoa. Tafiti za
kisaikolojia zinasema hujengwa katika mtazamo hasi. Baadhi ya hofu hizo ni kama
zifuatazo: -
©
Hofu
ya kutoridhishwa katika tendo la ndoa.
©
Hofu
ya kutomridhisha mmewe katika tendo la ndoa.
©
Hofu
ya mmewe kupotea hamu ya ndoa.
©
Hofu
ya mmewe kumkinai na kuanza michepuko.
©
Hofu
ya mmewe kutobadilika katika baadhi ya matendo yasiyompendeza.
©
Hofu
ya kutokua kiroho kama wanandoa.
Naomba
nifafanue kidogo juu ya hofu hizo sita hapo juu.
©
Hofu ya kutoridhishwa katika tendo
la ndoa na mmewe.
Kutokana
tafiti na ushahidi wa kimazingira ndoa nyingi zinazofungwa sasa zinakutanisha
wanandoa wenye uzoefu wa viwango tofauti wa tendo la ndoa ambao wameupata kwa
wanaume wengine tofauti na mme anayefunga nae ndoa. Hii inatokana na jamii
kukosa maadili ya ki-utamaduni na kidini upande wa malezi.
Wanawake
wengi wanaingia katika ndoa kwa kufuata hali ya uchumi ya muoaji au kutokana na
umri kuwatupa mkono na hivyo kujiingiza katika ndoa na shinikizo hizo mbili,
kwa sababu wenye kukidhi haja za tendo la ndoa hawahitaji kuwaoa au ni waume wa
watu. Kutokana na uzoefu wa kukutana na wanaume mbalimbali na wengi kutokidhi
haja zao za tendo la ndoa huingia katika ndoa na hofu hii. Tafiti zinaonyesha
kwamba mwanamke akitembea na wanaume kumi ni mmoja au sifuri wenye uwezo
wakumridhisha katika tendo la ndoa. Na hii ndio inayowafanya kuingia katika
ndoa na hofu hiyo, licha ya kwamba asilimia kubwa ya ndoa za siku hizi wanandoa
wengi huingia kwenye ndoa wakiwa wanajuana vizuri. Lakini huingia kwenye ndoa
kwa kutegemea kwamba wenza wao
watabadilika na kuweza kuwaridhisha kadri watakavyoendelea kuishi.
©
Hofu ya kutomridhisha mmewe katika
tendo la ndoa.
Kama
nilivyongea kwenye kipengele cha hapo juu ya uzoefu wa kufanya tendo la ndoa
kabla ya ndoa. Pamoja na uzoefu wa kuachwa na wanaume mbalimbali zikiambatana
na kashfa mbalimbali kutoka kwa wanaume waliyowaacha huwajengea hofu ya kukidhi
haja ya waume zao ya tendo la ndoa. Na kwa wanandoa ambao hawaongelei kabisa
juu ya tendo hilo na hawana maandalizi kabla na tendo la ndoa huishi katika
hofu hiyo maisha yao yote.
Hii ni changamoto
kubwa sana katika ndoa nyingi dunia nzima, ndio talaka zinazidi kuongezeka.
©
Hofu ya mmewe kupoteza nidhamu ya
ndoa.
Kawaida
ukiwa katika ndoa kuna nidhamu ambayo lazima izikatiwe kama vile muda wa kurudi
nyumbani, matumizi, ulaji nakadhalika kwa ndoa ambazo wanandoa wanaheshimiana.
Katika ndoa ambayo wanandoa wanheshimiana kila mmoja ni mlinzi wa mwenzie yaani
kuagana na kujulishana kila mmoja alipo inakuwa ni jambo la kawaida kabisa.
Kutokana na
ndoa nyingi kupoteza nidhamu mme kulala nje, kuchelewa kurudi nyumbani n.k. wanawake
wengi huwa na hofu ya ndoa zao kuingia katika misukosuko ya aina hii.
©
Hofu ya mmewe kumkinai na kuanza
michepuko.
Kutokana na
hofu ya kutokumridhisha mmewe hofu ya kukinaiwa na mmewe hujitokeza.
©
Hofu ya mmewe kutobadilika katika
baadhi ya matendo yasiyompendeza.
Kutokana na sababu ya kuingia kwenye
ndoa kutokana shinikizo nilizozitaja hapo juu, wanandoa wengi hugundua kwamba
wenzio wao mara nyingine wanatabia ambazo ni kero kama vile ubishi, uchelewaji
kurudi nyumbani bila taarifa, kufanya mambo ya msingi bila kumshirikisha
mwenza, kutopenda kula nyumbani n.k. Mambo haya kimsingi huleta msongo wa
mawazo pale ambapo mme anaambia kujirekebisha lakini anakuwa mgumu kubadilika
kwa sababu ya tabia za mfumo dume.
©
Hofu ya kutokua kiroho kama
wanandoa.
Katika nchi hasa za ki-afrika kuna
ndoa za aina tatu(3):
ü Kiserikali
ü Kimila
Tafiti zinaonyesha kwamba ndoa
nyingi zinafungwa kidini, kutokana na hofu nilizozitaja hapo juu suluhisho
pekee linategemea imani ya wahusika. Hili kutatua matatizo hayo hapo hali ya
imani ya kidini ya wanandoa ni muhimu sana kwa maana taasisi hii mwanzilishi ni
Mungu mwenyewe kwa mujibu vitabu vya kidini. Kwa hiyo, Imani inapokuwa chini ni
vigumu sana kutatua hofu zinazojitokeza katika taasisi hii muhimu sana.
Nimeongea kifupi kwenye kila
kipengele na ninaamini kila jambo linasuluhisho katika dunia hii. Naomba nipate
maoni yenu.
No comments:
Post a Comment