Sunday 6 November 2016

MIGOGORO YA NDOA NA TOFAUTI YA KIJINSIA


Ziko tofauti nyingi za kijinsia kati ya wanawake na wanaume, ambazo mara nyingi zimekuwa chanzo cha migongano, migogoro na mivutano katika ndoa. Kutokuzifahamu tofauti hizi kumesababisha wanandoa kupeana upendo ambao kila mmoja angependa apatiwe, badala ya upendo ambao mwenzake angependa apatiwe yeye, kulingana na silika ya jinsia yake.
Mara nyingi wanawake wamewapa wanaume malezi ya kuwajali, badala ya malezi ya kuonyesha kuwa na Imani nao. Wakati huo huo, wanaume wamewapa wanawake malezi kuonyesha kuwa na Imani nao, badala ya malezi ya kuwajali. Kutokana na mpishano huu, ndoa nyingi zimejikuta katika mivutano mingi, na changamoto ya kutokuridhishana, kwa pande zote mbili.
Utakuta, kwa vile mahitaji ya mwanamke ya msingi ya hisia za moyo ni mwenzi wake kumjali, basi anafikiri ndiyo mahitaji ya msingi ya mwanaume pia. Vivyo hivyo, utakuta mwanaume anataka mpenzi wake aonyeshe kuwa na imani naye. Hivyo, anajaribu kutoa mapenzi ya kuonyesha kuwa na Imani kwa mwenzi wake hitaji ambalo yeye angependa apatiwe na huyo mwenzi wake. Kila mmoja, pasipo kujua, anatoa aina ya mapenzi ambayo yeye angependa apatiwe, badala ya mapenzi ambayo mwenzi wake angependa apatiwe, kutokana na tofauti ya kijinsia aliyonayo.
Kwa kuelewa tofauti hizi za jinsia, na kwa kujitahidi kuuweka ufahamu huo katika matendo, misuguano iliyoko katika ndoa kati ya wanawake na wanaume itaweza kupungua kwa kiasi kikubwa. Ingawa hii pekee yake haitoshi kumaliza mivutano na migogoro katika ndoa, lakini ni moja ya njia muhimu ya kuboresha mahusiano katika ndoa.
Kuna wanandoa ambao, hata pasipo ufahamu huu, wameweza kuchukualiana na kuishi pamoja kwa mafanikio, na kuweza kuoanisha tofauti hizi za kijinsia. Hii ni kutokana na kipawa na alichonacho mmojawapo au wote wawili, katika kuoanisha tofauti hizi. Lakini, kufanikiwa huku pasipokuwa na ufahamu huu kunatokana  na kipawa cha kuzaliwa.
Lakini hata kama mtu anacho kipawa cha kuzaliwa, kukiboresha kupitia kuongeza ufahamu ni jambo la msingi. Hata kama ndoa ni bora, siku zote kuna nafasi ya kuzidi kuboresha zaidi na zaidi kupitia kuongeza ufahamu kuhusu ndoa. Maarifa siku zote ni silaha. Yaani maarifa yanampa mtu uwezo wa kutawala jambo.
Dr. Abraham Maslow, mwanasaikolojis mashuhuri wa karne ya ishirini, anaeleza kuhusu ufahamu na maarifa, kama ifuatavyo;
Elimu, ujuzi, ufahamu, kuijua kweli, na udhihirisho ni tiba ya hali ya juu…….na kama     ufahamu unatibu, basi kukosa ufahamu kunasababisha kuugua.
Maarifa, ufahamu, ujuzi au elimu ni silaha muhimu sana kwa binadamu, silaha ambayo ikimpa kudhibiti mambo, na kutawala changamoto mbalimbali katika maisha yake. Na katika ndoa pia, maarifa yanayohusu ndoa ni moja ya mhimili muhimu.

Ili kupata makala hizi kwenye barua pepe yako jaza kisanduku hicho pembeni mkono wa kulia.

Monday 17 October 2016

NGUZO KUMI ZA MWANAUME BORA ALIYEOA

Habari za majukumu mbalimbali ya kiuchumi ndugu wasomaji wa blogu hii, bila shaka nyote ni wazima kwa uweza wa mwenyezi Mungu muumba mbingu na nchi. Kwa wale ambao afya zao zimetetereka kidogo Mungu yu pamoja nanyi mtapona.
Leo napenda kutaja mambo kumi muhimu katika kudumisha mahusiano ya aina yote lakini hasa ndoa na uchumba: -
1. Mungu.
2. Upendo.
3. Roho.
4. Kujitolea
5. Agano.
6. Kukubaliana.
7. Mawasiliano.
8. Kusameheana.
9. Kujitawala.
10. Kuwa msaada kwa mwenza wako.

Ufafanuzi wa kina wa kila kipengele unapatikana kwenye blogu ya http://mkombozi-mahusiano.blogspot.com ambayo gharama yake ya kujiunga uwanachama ni TZS. 10,000.00 kwa Airtel Money 0784190882 au TiGO pesa 0719841988. Blogu hii imeshehena makala mbalimbali kuhusiana na mbinu za kujenga na kuboresha mahusiano. Fanya uamuzi hutajutia uamuzi wa kujiunga na blogu husika.

Karibu kwenye makala ijayo na waalike na wenzio, ili uendelee kupata maarifa ya kuimalisha na kuboresha mahusiano.

Monday 10 October 2016

MAMBO YANAYOATHIRI MALEZI YA WATOTO

Napenda tena kuchukua nafasi hii adimu kumshukuru Mwenyezi Mungu muumba wa mbingu na nchi kwa kunipa nafasi ya kuwasilisha kwenu makala ya mambo manne (4) yanayoathiri makuzi ya watoto. Pia napenda kuwashukuru wale wote waliopata nafasi ya kusoma makala zangu kwa maoni na mawazo yenu mazuri, napenda kuchukua nafasi hii kuwaombeni mwaalike na wenzenu kusoma makala zangu ambazo natoa kila wiki.
Katika hali inayokubali katika jamii zetu, mtoto ni matokeo ya wawili waliyokubaliana kuishi kama mke na mme baada au kabla ya kufunga ndoa. Japo mara nyingine watoto wanapatikana pasipo na lengo la kufunga ndoa. Leo niongee mambo manne (4) yanayoathiri makuzi ya mtoto kwa ujumla.
Makuzi ya mtoto/watoto ni jukumu la muhimu sana kwa mzazi yo yote katika jamii.

Katika tafiti mbalimbali za kisayansi makuzi anayopata mtoto kuanzia umri wa miaka 0 hadi 12 yanaakisi tabia atakayokuwa nayo katika utu uzima wake. Mambo 4 yafuatayo yanayoathiri makuzi ya mtoto ni kama yafuatavyo: -
1. Kuadibisha: Hatua za kinidhamu unazochukua dhidi ya mtoto wako huathiri malezi yake. Wataalam wa malezi ya watoto wanashauri malezi yetu yawe shirikishi kwa maana ya kwamba kila unapomkataza mtoto kufanya jambo fulani kama vile kutukana watu, utoro shuleni, ugomvi n.k ni vizuri zaidi ukawa unamfahamisha ni kwa nini haifai kufanya jambo fulani, ili kumpatia nafasi ya kuhoji/kutafakari/kuelewa badala ya kumshurutisha tu kutekeleza maagizo. Kwa kufanya hivyo, unampa uwezo wa kupambanua, kuelewa na kujiamini katika maamuzi mbalimbali. Pia hatua kali za kinidhamu kama vile kumchapa mtoto zinaweza kusababisha hofu kwa watoto wako, ambayo huathiri uwezo wao wa kuwasiliana na wewe, walimu hata wenzao pia. Hata hivyo, pia haitakiwi kuwa mpole mno kwa sababu watoto wanaweza kuendelea kwa wakosefu wa nidhamu na kuathiri mwenendo wao katika jamii na shuleni.
2. Mazingira: Neno mazingira kwa tafsiri fupi ni vitu vyote vinavyotuzunguka hewa, miti, majengo, watu, wanyama, shule, nyumba za ibada .n.k. Mazingira ya mtoto yanaathiri ya moja kwa moja kwa mtoto hasa ya nyumbani na shuleni. Muda mwingi wa makuzi ya watoto hutumika nyumbani na shuleni. Mtoto anayetoka kwenye nyumba ambayo wazazi wake wako katika hali ya ugomvi kila mara, umasikini, utajiri n.k. mambo hayo uathiri moja kwa moja utazamo wa mtoto wa kimaisha. Pia mtoto ambaye anasoma shule ambayo kila saa anakosa amani kutokana na kutishiwa kupigwa na walimu au wanafunzi wenzie hujengewa hali ya kuwa na wasiwasi na kutopenda kwenda shuleni na shule.
3. Mawasiliano: Mtoto ashirikishwe katika baadhi ya maamuzi ya ki-familia kama vile masuala ya chakula, vinywaji, maongezi n.k. Ninaposema kushirikishwa katika suala ya chakula ni katika hali ya kujenga tabia ya ushirikishwaji na kumpa uhuru wa maamuzi kumuuliza mtoto leo unataka kula nini mama/baba ni kuonyesha kuthamini mawazo yake. Pia katika maongezi nina maana mtoto sema jambo lo lote ni muhimu kumsikiliza na siyo vizuri kumpuuza au kumkaripia kwamba anapiga kelele. Tabia hiyo, itamsaidia kwa kumpatie uwezo wa kujieleza na kujisikia kuthaminiwa na wazazi wake.
4. Malezi: Mfumo wako wa malezi unaweza kumjenga mtoto wako au kumharibu. Kuweka ratiba ya kukaa na watoto na kuongea nao na kusikiliza mawazo hayo huwajengea hali ya kujisikia kuathaminiwa na kupendwa na wazazi/walezi na hivyo kuwaongezea furaha na amani. Pia tabia hii huwajengea hali ya kujiamini na uhuru wa kueleza hisia zao nyumbani na shuleni bila hofu kwa sababu ya Imani ya kupendwa imejengwe kwenye akili zao.
Kwa hiyo, wazazi tuna jukumu kubwa sana katika kujenga watoto wetu kisaikologia katika umri wa miaka 0 hadi miaka 12. Kumjenga mtoto baada ya miaka 12 na kuendelea inakuwa vigumu sana, japo inaweza kumbadilisha.
Jiunge na blog ili upate kila makala ya blog hii.


Friday 7 October 2016

MATARAJIO YA WANANDOA KWENYE MAISHA YA NDOA

Karibuni ndugu wasomaji wa mara kwa mara wa wavuti na wale ambao ni mara ya kwanza wameingia kwenye wavuti.

Wanandoa huwa na matarajio mengi sana katika maisha yao ya ndoa hasa matarajio mazuri daima.  Maisha ya ndoa ni mchakato ambao hupita katika hatua kuu nne (4) yaani; kuzaliwa, kukua, kuzeeka na kufa. Lakini si ndoa zote hupitia hatua hizo zote nne (4) baadhi hupitia hatua tatu (3) au mbili (2) kutokana na baadhi ya wanandoa kuacha kumkabidhi mlezi na mwanzilishi wa ndoa duniani yaani; Mungu. Kwenye makala hii, sitaki kuongelea sababu anuai zinazosababisha baadhi ya ndoa kutopitia hatua kuu nne (4) mzunguko wa maisha ya ndoa. Baadhi ya matarajio maisha ya iliyo katika hatua ya pili (2) ni kama yafuatavyo:-

ü  Changamoto za masuala ya kifedha.

ü  Changamoto za kimawasiliano baina yao.

ü  Changamoto zinazoletwa na wanandugu na watoto.

ü  Upweke.

ü  Kukua/kudumaa kiroho.

ü  Migogoro.

ü  Magonjwa.

Kipengere cha 4 hadi 7 nitavifafanua lakini cha 1 hadi 3 zilishavifanunua kwenye makala zangu za awali za changangamoto zinazosababishwa na wanandoa wenyewe na changamoto zinazosababishwa watu wengine wasiyowanandoa.

Upweke; Kutokana na kuongezeka kwa majukumu na uwajibikaji kwa masuala ya kifamilia maisha uliyokuwa unategemea kuwa yatakuwa daima ya amani na furaha huanza kubadilika na hapo ndipo hali ya kutaka kukaa kiupweke uanza kujitokeza ili kutafari zaidi majukumu ya kifamilia na hamu ya tendo la ndoa hupungua kwa sababu ubongo unakuwa umezingirwa na mawazo ya namna ya kutatua majukumu yaliyo mbele kama vile ada, kodi ya nyumba, gharama za usafiri kwenda na kurudi kazini, chakula nakadhalika.

Migogoro; Kutokana ndoa kuwa katika hatua ya kukua  tabia zote zilizokuwa zimevichwa na wanandoa wote uanza kudhihirika kwa sababu tabia haiwezi kufichwa daima. Tabia za kiburi, jeuri, dharau, hasira, uasherati nakadhalika uanza kuonekana na kuleta migogoro ya hapo pale katika ndoa. Hatua hii inahitaji busara na hekima kubwa hasa kwa kumshirikisha Mungu, ili kuweza kuivuka na ndoa nyingi sana huishia hatua hii.

Magonjwa; Kwa sababu za kimazingira na vyakula imekuwa ni jambo la kawaida kwa binadamu kuugua kwa muda mrefu au mfupi. Inapotokea uuguaji ni wa muda mrefu jambo ili uyumbisha sana hali ya uchumi wa wanandoa na kama hakuna upendo wa dhati basi hata misingi ya ndoa uanza kulegalega.

Mwacheni Mungu awe mtawala katika maisha yenu ya ndoa kwa maana yeye ndie muasisi ya taasisi ya ndoa hakika ndoa yenu itadumu na itakuwa kisima cha amani na furaha. Na pia nakushauri ujiunga na blogu ya http://mkombozi-mahusiano.blogspot.com bure.

Jiunge na blogu tajwa hapo UPATE MAARIFA YA KUPUNGUZA MIGOGORO KATIKA MAHUSIANO, TUJENGE TAIFA IMARA.

 

 

 

 

 

Saturday 14 May 2016

NJAA MBILI (2) ZINAZOWASUMBUA WANADOA KATIKA MAISHA YAO YA NDOA


Habari rafiki na mpenzi msomaji wa wavuti hii. Na karibu tena katika makala yetu ya leo ili tuweze kujifunza. Katika makala yetu ya leo tutajifunza njaa zinazowasumbua wanandoa katika maisha yao ya ndoa. Kuzifahamu njaa zinazowasumbua wanandoa tafadhali twende sanjari mpaka mwisho wa makala hii.

Kumekuwa na mitazamo hasi sana juu ya maisha ya ndoa. Kabla mtu hajaingia ndani ya maisha ya ndoa tayari akili yake imeshajazwa mitazamo hasi juu ya maisha ya ndoa. Mtu aliyepatwa na matatizo katika maisha yake ya ndoa naye atakwenda kuwaaminisha watu juu ya matatizo yake juu ya ndoa. Siyo kwamba katika maisha ya ndoa hakuna changamoto la hasha zipo kama kawaida kama vile kwenye kazi, biashara, ujasiriamali nakadhalika. Hivyo kwenye jambo lolote changamoto haziepukiki. Kweli itakuweka huru na usipoujua ukweli utapata shida sana. Maisha ya ndoa unayotaka kuishi unayatengeneza wewe mwenyewe na si vinginevyo hivyo usipoteze muda wa kuhangaika tengeneza yale maisha ambayo unayataka kuishi na usisikilize kelele za watu ambazo zitakuwekea ukungu katika macho yako na kushindwa kuona mbele. Na waswahili wanasema ukiona vyaelea ujue vimeundwa kwa hiyo, hata wewe unaweza kuviunda katika maisha yako ya ndoa.

Katika hali ya kawaida hakuna mtu asiyeijua njaa, mtu akiwa na njaa anapoteza kabisa nguvu na hata ufanisi wa kazi aliyokuwa anafanya unapotea, kwa hiyo njaa huwa inalegeza watu kama akikosa kula chakula na kushiba. Vivyo hivyo, kila mwanandoa ana njaa yake yaani mwanaume ana njaa yake katika maisha ya ndoa hali kadhalika kwa mwanamke naye ana njaa yake. Kwa maana hiyo, kila mwanandoa anahitaji ashibishwe njaa yake na mwenza wake. Ikitokea sasa wanandoa hao yaani wawili hao kutoshibishana njaa zao ndio matatizo huanzia hapo. Na tunajua ya kwamba wawili hao kila mmoja ana njaa yake. Hivi ikitokea mtu ana njaa ya chakula halafu pale anapotegemea kupata chakula ili ashibishe njaa yake hapati ataendelea kusubiri kubaki na njaa yake? Jibu ni kwamba lazima atatafuta sehemu ambayo ataweza kupata chakula ili aweze kushibisha njaa yake.
Ndugu msomaji, kama kila mwanandoa ameshindwa kumshibisha mwenzake basi ujue lazima atatafuta chakula sehemu nyingine ili kuweza kukidhi njaa yake. Hivyo basi, kumbe ni wajibu wa kila mwanandoa kuhakikisha anamshibisha mwenzake njaa yake.

Zifuatazo ni njaa mbili zinazowasumbua wanandoa endapo hawatashibishana;


1. Njaa ya mwanamke ni upendo;


Mwanamke anahitaji upendo kuliko vitu vingine, hata katika vitabu vya dini vinasema; enyi waume, wapendeni wake zenu. Ampendaye mkewe hujipenda mwenyewe, mwanaume anatakiwa kujitoa kwelikweli kumpenda mke wake kama tunavyojua upendo ndio falsafa kubwa sana katika maisha ya binadamu, upendo huvumilia, hufadhili, hauhusudu. Hivyo basi njaa ya mwanamke ni kupendwa. Wewe kama mwanaume unatakiwa kumpenda mke wako kwa moyo wako wote bila kujali udhaifu wake. Hii ndio njaa ya wanawake wanahitaji upendo katika maisha ya ndoa.

2. Njaa ya mwanaume ni kuheshimiwa;


Mwanaume njaa yake kubwa ni kuheshimiwa katika maisha ya ndoa. Sasa ikitokea mwanaume anakosa kuheshimiwa na mke wake katika maisha ya ndoa hivyo anakuwa amekosa kushibishwa njaa yake. Na kama akikosa kushiba ndio matatizo huanzia hapo itamlazimu kutafuta kushibishwa njaa yake nje. Hivyo kama wewe ni mwanamke unatakiwa kumshibisha mume wako njaa yake ya kumtii.

Kama wanandoa wanashindwa kushibishana njaa zao, hivyo wanajitengenezea shimo wao wenyewe. Watu wanajisahau sana katika kutimiza majukumu yao katika maisha ya ndoa hatimaye wanaruhusu haki za kibinadamu kuingia maisha ya ndoa, kama wanandoa mkishaingiza haki za kibinadamu katika maisha ya ndoa yaani hamsini kwa hamsini kama wanavyodai lazima mtapoteza mwelekeo tu. Kwa hiyo kila mtu ana njaa yake kama tulivyoona hapo juu sasa mkishayaingiza mambo haya ya kidunia mtakosa kushibishana njaa zenu.

Mwisho, kila mwanandoa ana wajibu wa kumshibisha mwenza wake, mke akipendwa atashiba njaa yake na mume akiheshimiwa atashiba njaa yake. Kila mtu ana njaa yake hivyo mnatakiwa kushibishana na kupendana katika shida na raha.
Makala hii imeandikwa na Deogratius Kessy ambaye ni mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali, unaweza kuwasiliana naye kupitia namba 0717101505 au kwa barua pepe deokessy.dk@gmail.com au unaweza kutembelea tovuti yake www.actualizeyourdream.blogspot.com

Tuesday 10 May 2016

JINSI UNAVYOWEZA KUMJENGEA MTAZAMO CHANYA MTOTO WAKO


Kuna msemo ‘usemao mtoto umleavyo ndivyo akuavyo’. Ni msemo ambao mara kwa mara huwafundisha wazazi umuhimu wa kulea watoto wao katika maadili mema na ya kimafanikio. Mara nyingi ikumbukwe kwamba wazazi huwa ndio wenye jukumu kubwa sana la kulea watoto wao tofauti na watu wengine kama walimu, madaktari na jamii, jukumu la kwanza huwa lipo kwa mzazi.

Hapa mzazi huwa ana kazi kubwa sana kumbuka tu si tu ya kumlea huyu mtoto katika mazingira hatarishi peke yake yatakayomdhuru, lahasha bali huwa ana jukumu pia la kuhakikisha mtoto huyu anakulia katika malezi bora ambayo yatampelekea awe na mtazamo chanya katika maisha yake siku zote.

Kwa mujibu wa wataalamu wa masuala ya walezi ya watoto wanadai kwamba msingi mkubwa wa maisha ya binadamu huwa unajengwa kuanzia miaka 0-12. Hiyo ikiwa na maana kama mtoto wako utamlea vizuri kwenye umri huu basi elewa atakuwa na nafasi kubwa ya kufanikiwa tofauti na yule ambaye atalelewa katika maadili mabovu.

Mpaka hapo unaweza ukawa umeona kwamba umri wa kuwa makini na mtoto wako ni umri huu ambao upo chini ya miaka 12. Katika umri huu, hapa wengi ndipo wanapoharibu au kutengeneza watoto wao. Kama unafikiri natania jaribu kufatilia wale watoto ambao wamevuka umri huu. Kwa tabia yoyote atakayokuwa nayo msingi wake mkubwa umetokea kwenye miaka 0-12.

Kwa kulifafanua hili vizuri, nikiwa na maana kama mtoto wako unaona ana tabia mbaya basi elewa kabisa ulimharibu tokea akiwa chini ya miaka 12 na wala usisingizie kitu chochote nje ya hapo. Na ndiyo maana ni hatari sana kwa mzazi kumpeleka mtoto wake chini ya umri huu shule za boarding kwa sababu huu ndiyo umri ambao mtoto anatakiwa apewe msingi bora wa maisha ikishindikana hapo basi tena.

Kwa hiyo kitu cha msingi katika umri ni kumpa mtoto malezi bora yatakamfanya ajitambue zaidi. Malezi haya kwa bahati mbaya tofauti na wengi wanavyofikiri hawezi kupewa na mwalimu au na mtu mwingine yoyote kwa ubora wa hali ya juu zaidi ya mzazi. Kwani ni kipindi ambacho unatakiwa umfundishe mtoto wako juu ya mambo mengi kama upendo, kujali, utunzaji mzuri wa fedha, utu, kuokoa muda, kutoa, kujiamini na mambo mengineyo mengi.

Kwa kukosa mambo hayo baadae hupelekea mtoto huyu kuanza kuteseka kujifunza upya na tena kwa tabu lakini kumbe wakati alitakiwa kujifunza akiwa mdogo tena kwa urahisi . kwa kulijua hili leo unaweza ukaanza na kumfundisha mtoto wako namna ya kumjengea mtazamo chanya ambao utamfanya ajiamini na kufanya vizuri katika kila eneo la maisha kwa ubora wa hali ya juu.

Je, unawezaje kumjengea moto wako mtazamo chanya?

1. Msifie.

Jijengee tabia ya kumsifia mtoto wako kwa yale mambo madogo anayoyafanya. Acha kumkosoa na kiasi cha kwamba kujiona hafai. Hakikisha unampa sifa. Sifa hizo itakuwa nzuri sana kama utakuwa unampa hadharani mbele ya wenzake. Hilo litamfanya ajiamini zaidi na kujiona yeye anaweza. Kwa kadri utakavyoendelea kumsifia atajikuta mtoto wako anazidi kuwa mwenye uwezo mzuri wa kujiamini sana.

 

 
MSIFIE MTOTO WAKO ANAPOFANYA JAMBO ZURI
 


2. Mwamini.

Mbali na kumpa sifa, lakini pia unaweza kumjengea mtoto wako tabia nzuri ya kujiamini kwa wewe kumwamini pia katika yale mambo anayofanya. Kama ni kazi umemwachia, mwache aifanye akiwa peke yake huku ukiwa unamfatilia sio sana ili kuona anafanyaje. Kwa kitendo cha kumfanyia hivyo atajiona kuwa yeye kumbe anaweza kufanya mambo makubwa na hivyo atajikuta akiwa anajiamini.

3. Mpe majina mazuri.

Weka utararibu wa kumpa mtoto wako majina mazuri yatakayomfanya ajiamini. Kila unapokutana naye mbali na kumuita jina lake halisi unaweza ukamuita ‘Pilot, shujaa, mshindi, mtaalamu’ na mengineyo mengi yatakamfanya ajiamini na kujiona bora kuliko. Epuka kumpa ‘lebo’ za kumuita majina kama vile ‘mjinga wewe, kichwa maji we’. Hiyo itamkatisha tamaa na itamfanya ashindwe kujiamini.

4. Mpe mazoezi ya kuongea mbele za wenzake.

Anapokuwa na wenzake tafuta kitu cha kuongea na kumfanya aongee mbele za wenzake. Hata kama anaona aibu mpe moyo wa kumfanya aendelee kuongea. Kwa kitendo hicho kitamfanya azidi kujiamini sana na itampelekea kweli kuongeza uwezo wake mkubwa wa kujiamini siku hadi siku. Hata wakati mwingine hata kuwa na ule woga mkubwa ndani yake wa kuzungumza.

Unaweza ukafanya mambo mengi yatakayomfanya mtoto wako azidi kujiamini. Lakini kwa leo fanyia kazi kwanza hayo na hakikisha mtoto wako anaweza kujiamini kwa namna yoyote ile. Hiyo itamsaidia sana kwa maisha yake yote ya baade.

Kwa makala nyingine nzuri pia tembelea DIRA YA MAFANIKIO kwa kujifunza na kuhamasika kila siku.

Ni wako rafiki katika mafanikio,

Imani ngwangwalu,

Simu; 0713 048 035,



 

Friday 29 April 2016

MWALIKO

Tembelea mara kwa mara mara wavuti hii: http://tumaini-mahusiano.blogspot.com

MAMBO SITA (6) YANAYOWATIA HOFU WANAWAKE KATIKA NDOA


Karibu ndugu wasomaji wa wavuti hii, leo napenda kuongelea mambo sita yanayowatia hofu wanawake kwa waume zao pamoja ustawi wa ndoa zao. Kutokana na tafiti mbalimbali na uzoefu wa kimazingira kuna hofu nyingi wanazokuwa nazo wanawake dhidi ya waume zao hasa kwa ndoa changa na ambazo hazikupitia hatua ya uchumba wa muda mrefu. Kama iliyohada mke na mme hukutana wakiwa wote ni watu wazima waliyokulia katika mazingira, utamaduni na familia tofauti wakapendana na kufikia maamuzi ya hiari ya kufunga ndoa. Kutokana na mzingira, makuzi, utamaduni, mtazamo n.k. watu wanapokuwa wameamua kufunga ndoa hutokea hofu za kimahusiano za hapa na pale ambazo kila mmoja hujitahidi kuziondoa. Tafiti za kisaikolojia zinasema hujengwa katika mtazamo hasi. Baadhi ya hofu hizo ni kama zifuatazo: -

©       Hofu ya kutoridhishwa katika tendo la ndoa.

©       Hofu ya kutomridhisha mmewe katika tendo la ndoa.

©       Hofu ya mmewe kupotea hamu ya ndoa.

©       Hofu ya mmewe kumkinai na kuanza michepuko.

©       Hofu ya mmewe kutobadilika katika baadhi ya matendo yasiyompendeza.

©       Hofu ya kutokua kiroho kama wanandoa.

Naomba nifafanue kidogo juu ya hofu hizo sita hapo juu.

©       Hofu ya kutoridhishwa katika tendo la ndoa na mmewe.

Kutokana tafiti na ushahidi wa kimazingira ndoa nyingi zinazofungwa sasa zinakutanisha wanandoa wenye uzoefu wa viwango tofauti wa tendo la ndoa ambao wameupata kwa wanaume wengine tofauti na mme anayefunga nae ndoa. Hii inatokana na jamii kukosa maadili ya ki-utamaduni na kidini upande wa malezi.

Wanawake wengi wanaingia katika ndoa kwa kufuata hali ya uchumi ya muoaji au kutokana na umri kuwatupa mkono na hivyo kujiingiza katika ndoa na shinikizo hizo mbili, kwa sababu wenye kukidhi haja za tendo la ndoa hawahitaji kuwaoa au ni waume wa watu. Kutokana na uzoefu wa kukutana na wanaume mbalimbali na wengi kutokidhi haja zao za tendo la ndoa huingia katika ndoa na hofu hii. Tafiti zinaonyesha kwamba mwanamke akitembea na wanaume kumi ni mmoja au sifuri wenye uwezo wakumridhisha katika tendo la ndoa. Na hii ndio inayowafanya kuingia katika ndoa na hofu hiyo, licha ya kwamba asilimia kubwa ya ndoa za siku hizi wanandoa wengi huingia kwenye ndoa wakiwa wanajuana vizuri. Lakini huingia kwenye ndoa kwa  kutegemea kwamba wenza wao watabadilika na kuweza kuwaridhisha kadri watakavyoendelea kuishi.

©       Hofu ya kutomridhisha mmewe katika tendo la ndoa.

Kama nilivyongea kwenye kipengele cha hapo juu ya uzoefu wa kufanya tendo la ndoa kabla ya ndoa. Pamoja na uzoefu wa kuachwa na wanaume mbalimbali zikiambatana na kashfa mbalimbali kutoka kwa wanaume waliyowaacha huwajengea hofu ya kukidhi haja ya waume zao ya tendo la ndoa. Na kwa wanandoa ambao hawaongelei kabisa juu ya tendo hilo na hawana maandalizi kabla na tendo la ndoa huishi katika hofu hiyo maisha yao yote.

Hii ni changamoto kubwa sana katika ndoa nyingi dunia nzima, ndio talaka zinazidi kuongezeka.

©       Hofu ya mmewe kupoteza nidhamu ya ndoa.

Kawaida ukiwa katika ndoa kuna nidhamu ambayo lazima izikatiwe kama vile muda wa kurudi nyumbani, matumizi, ulaji nakadhalika kwa ndoa ambazo wanandoa wanaheshimiana. Katika ndoa ambayo wanandoa wanheshimiana kila mmoja ni mlinzi wa mwenzie yaani kuagana na kujulishana kila mmoja alipo inakuwa ni jambo la kawaida kabisa.

Kutokana na ndoa nyingi kupoteza nidhamu mme kulala nje, kuchelewa kurudi nyumbani n.k. wanawake wengi huwa na hofu ya ndoa zao kuingia katika misukosuko ya aina hii.

©       Hofu ya mmewe kumkinai na kuanza michepuko.

Kutokana na hofu ya kutokumridhisha mmewe hofu ya kukinaiwa na mmewe hujitokeza.

©       Hofu ya mmewe kutobadilika katika baadhi ya matendo yasiyompendeza.

Kutokana na sababu ya kuingia kwenye ndoa kutokana shinikizo nilizozitaja hapo juu, wanandoa wengi hugundua kwamba wenzio wao mara nyingine wanatabia ambazo ni kero kama vile ubishi, uchelewaji kurudi nyumbani bila taarifa, kufanya mambo ya msingi bila kumshirikisha mwenza, kutopenda kula nyumbani n.k. Mambo haya kimsingi huleta msongo wa mawazo pale ambapo mme anaambia kujirekebisha lakini anakuwa mgumu kubadilika kwa sababu ya tabia za mfumo dume.

©       Hofu ya kutokua kiroho kama wanandoa.

Katika nchi hasa za ki-afrika kuna ndoa za aina tatu(3):

 ü  Kidini

ü  Kiserikali

ü  Kimila

Tafiti zinaonyesha kwamba ndoa nyingi zinafungwa kidini, kutokana na hofu nilizozitaja hapo juu suluhisho pekee linategemea imani ya wahusika. Hili kutatua matatizo hayo hapo hali ya imani ya kidini ya wanandoa ni muhimu sana kwa maana taasisi hii mwanzilishi ni Mungu mwenyewe kwa mujibu vitabu vya kidini. Kwa hiyo, Imani inapokuwa chini ni vigumu sana kutatua hofu zinazojitokeza katika taasisi hii muhimu sana.

Nimeongea kifupi kwenye kila kipengele na ninaamini kila jambo linasuluhisho katika dunia hii. Naomba nipate maoni yenu.

 

 

 

 

 

 

 

Thursday 28 April 2016

UMUHIMU WA KUWA NA FAMILIA BORA ILI KUJENGA JAMII BORA.


Habari mpenzi msomaji wa wavuti hii? Na karibu katika makala yetu ya leo ambapo leo tutajifunza umuhimu wa kuwa na familia bora ili kujenga jamii bora. Bila familia bora hakuna jamii bora ambayo italeta maendeleo katika dunia. Tunapenda kujifunza mambo ya familia au tunasoma mambo ya familia kwa sababu kuu mbili;
Kwanza, sisi sote tumezaliwa katika familia. Hakuna mtu hapa duniani ambaye hajazaliwa katika familia ndio maana sisi sote tumezaliwa katika familia na tunapaswa kujifunza sana mambo ya familia.
Pili, familia ni msingi wa maisha ya mtu. Kila mtu anapata msingi wa maisha kutoka katika familia yake. Baba na mama wakimpatia mtoto msingi mzuri wa maisha yake basi mtoto atakwenda kujenga jamii iliyo bora kabisa. Ndio maana watu wako tofauti sana hii ni kutokana na kila mtu amepata msingi wa maisha tofauti na kuna wengine wamepata msingi mzuri wengine wamepata msingi mbaya.


Kwa kawaida familia inajengwa na baba, mama na watoto au mtoto. Familia ni kiungo cha msingi katika jamii. Mungu amepanga kila mtu kuzaliwa katika familia. Mtoto anajenga maadili na mtazamo wake kuhusu yeye mwenyewe, ulimwengu na maisha kutoka katika familia kulingana na mazingira alipozaliwa na alipokulia.
Ili tujenge jamii bora tunatakiwa kwanza tujenge familia bora kwa sababu kila mtu ametokea katika familia. Ndani ya familia baba na mama wanapaswa kuwafundisha watoto maadili mema tokea wakiwa wadogo kuwa mafunzo ya jinsi kuishi, kuwa na maadili mazuri. Mtoto akikosa kupewa upendo katika familia na kufundishwa falsafa hii kubwa ya upendo atakwenda kutengeneza jamii mbovu kama mtoto anatoka katika familia ambayo baba na mama wanaishi maisha ya uadui, ugomvi yaani kama vile maisha ya chui na swala. Mtoto anaona baba na mama wanapigana tokea akiwa mdogo je unafikiri anajenga nini katika akili yake? Baba ni mlevi wa kupindukia, wazazi wote wawili wanakosa upendo, hawaheshimiani wanatukanana mbele ya watoto, nyumba haina amani kila mtu na mambo yake matokeo yake wazazi wanapandikiza chuki kwa watoto matokeo yake ni kujenga jamii mbovu.
Familia ikiishi katika falsafa ya upendo tutajenga jamii bora yenye upendo. Upendo wa kujipenda wewe mwenye na watu mwingine. Familia ikikosa kuishi katika msingi imara wa upendo wanakwenda kujenga jamii ambayo haina hofu na mtu ambaye hana hofu atafanya kitu chochote anachojisikia na kuleta madhara makubwa kwa jamii. Kutokua na upendo hakuna huruma ya Mungu watu wanatenda mambo ya ajabu ambayo chanzo chake ni kukosa msingi bora kutoka katika familia.
Familia inayowajibika katika kufanya kazi kwa bidii, kila mmoja kutekeleza wajibu wake bila shuruti itajenga jamii bora. Familia kuwafundisha watoto kuwajibika ni mafanikio ya familia kuongeza kizazi kingine bora ambacho ndio jamii. Bila familia hakuna jamii. Jamii inapata faida kupitia familia, jamii inapata watu wanaowajibika kutoka katika familia. Familia ni mali ya jamii. Familia ikiwa nzuri na jamii itakua nzuri. Hivyo basi, familia ikiharibika na jamii inaharibika.
Watoto wanaathirika sana kisaikolojia wakiangalia matendo mabaya kutoka kwa wazazi. Mwisho wa siku watoto wanawachukia wazazi kwa matendo yao , watoto wanakata tamaa ya maisha na kuona hakuna sababu ya kuishi je kama familia imejengwa kwa msingi kama huu tutatengeneza jamii iliyo bora?

Mtu anafahamika katika jamii kama mtu wa familia fulani. Mtoto wa familia fulani na mzaliwa wa sehemu fulani. Kwa hiyo, familia inakuwa chanzo cha kujenga maisha ya mtu na familia ni muhimu sana katika malezi.
Makala hii imeandikwa na Deogratius Kessy ambaye ni mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali, unaweza kuwasiliana naye kupitia namba 0717101505 au kwa barua pepe deokessy.dk@gmail.com au unaweza kutembelea tovuti yake www.actualizeyourdream.blogspot.com

10 Simple Steps to Change Your Eating Habits - For Dummies

10 Simple Steps to Change Your Eating Habits - For Dummies

Monday 25 April 2016

MCHAKATO WA KUPATA MCHUMBA mwendelezo



Habari za siku nyingi ndugu zangu wasomaji wa wavuti hii. Samahani sana kwa ukimya wa muda mrefu sana, kwa sababu ni siku nyingi sana nimeanza makala hii, naomba leo niimalize kwa kuiongelea kwa kifupi ili tuendelea na makala zingine. Michakato inayofuatia ni kama ifuatavyo: -

4.      Kumshukuru Mungu

Ki-imani tunaamini kwamba mke/mme mtu hupewa na Mungu hasa kama umemshirikisha/ulimuomba kama mchakato unavyoeleza hapo juu. Na hii, ni kwamba kuoa/kuolewa ni mpango wa Mungu wa kuongeza kizazi cha wanadamu.

5.      Msichana/Mwanamke kuwajulisha wazazi wake 

Baada ya kumshukuru Mungu na kuafikiana kwenda kuwajulisha wazazi juu ya azma ya kuwa mke na mme hatua inayofuta ni msichana/mwanaume kwenda kuwajulisha wazazi juu ya suala la kumpata mwenza.

6.      Mvulana/mwanaume kwenda kwa wazazi wa mwanamke kuchumbia

Hatua ya mwisho ni wazazi wa mvulana/mwanaume kwenda kwa wazazi wa msichana/mwanaume kwenda kuchumbia ili hatimaye waweze kufunga ndoa.

Naomba nipate maoni yenu kuhusu makala husika.