Thursday 5 April 2018

MIGOGORO KATIKA NDOA NA MAHUSIANO


Kama nilivyoeleza kwenye makala yangu ya changamoto zinazosababishwa nawanadoa wenyewe mmojawapo ni mawasiliano(kutokuelewana). Hii ndio changamoto kubwa sana katika ndoa na ndio chanzo cha taraka nyingi kwa mujibu takwimu za kimataifa. Kwa bahati mbaya tarakwimu za hapa kwetu nimeshindwa kuzipata kwa njia ya vyanzo rasmi vya vinavyohusika na takwimu.


Kimsingi ni kwamba migogoro inayosababishwa na kutoelewana chanzo chake kinaweza kuwa ni mmoja wa wanadoa au wote wawili. Migogoro kikawaida ipo kwenye ndoa zote ila hutofautiana kwa kiwango. Ipo kwenye kila ndoa kutokana na sababu za malezi na tabia za asili za wanandoa. Na kawaida migogoro ukua kutokana na kukosa utayari wa kuitatua kwa wanandoa wenyewe ama kwa wote wawili au mmoja wao. Inapotokea hakuna utayari kwa wote wawili, ndoa haiwezi kudumu na kama ni kwa mmoja wao tu kuna asilimia fulani ndoa kuweza kudumu na kama wote wako tayari kutatua ndoa hii inakuwa na asilimia 100 kudumu.


Kama nilivyoongea kwenye makala tajwa hapo juu. Migogoro ya kutoelewana ipo inayotokana na mahitaji ya kawaida na ya kimwili. Leo tutaongelea migogoro inayotokana na mahitaji ya kawaida ya kimwili. Ninavyosema mahitaji ya kawaida nina maana mahitaji ya msingi ya binadamu kama vile chakula, mavazi na mahitaji mengine ambayo siyo msingi yaani; mahitaji ya kumpendezesha mwanandoa, kushaurishwa, kuthaminiwa n.k.


NAMNA YA KUPAMBANA NA MIGOGORO INAYOTOKANA NA MAHITAJI YA KAWAIDA


1.    Kuwa mkweli kuhusu hali ya kipato chake.


Kuwa mkweli wa hali yako ki-uchumi yaani; kuwa mkweli kwa mwenza wako kuhusu hali ya mapato yako. Na ukweli huu ni vizuri ufanyike kabla ya kufunga ndoa. Ni vizuri sana kama utauvaa uhalisia wako kipato kipindi chote cha uchumba. Hili, ni muhimu sana kwa sababu nitakusaidia kujua kama mchumba wako ni wa kiwango chako au la. Ukidanganya katika suala hili unakuwa umepande mgogoro ambayo itakuwa vigumu kuusuluhisha na unakuwa umejenga hali ya kutoaminika.


2.    Onyesha kujali hitaji la mwenza wako.


Jitahidi kujali mahitaji ya mwenza wako kwa kumtimizia hitaji lake kama uwezo unaruhusu na kama unaona sihitaji la msingi, tafuta lugha nzuri ya kumweleza ni kwa nini unaona hitaji lisitimizwe na bila kuonyesha dalili za kupuuza au kuonyesha sihitaji la msingi.


3.    Epuka kuonyesha upendeleo katika kusaidia ndugu.


Katika familia zetu za ki-afrika kuna matatizo ya kila namna kwenye familia zetu yaani; kwa upande wa mke na mwanaume. Inapotokea kuna mahitaji upande wa familia za upande mmojawapo ni muhimu sana kuweka uwiano wa misaada inayotolea, ili kuepuka kuonyesha upendeleo.


4.    Epuka kuonyesha upendeleo kwa wageni wanao watembelea nyumbani.

Ni jambo la kawaida sana ndugu wa pande zote kutamani kuwatembelea wanandoa katika hali ya amani au matatizo. Ni vizuri kujitahidi kutoonyesha unyanyapaa kwa wanandugu wa upande mmoja hali hii inaweza kuleta mgogoro mkuu.


5.    Epuka kuonyesha dharau dhidi ya mila na desturi za mwenza wako.


Inapotokea wanandoa ni makabila tofauti ina maana watakuwa wamekulia kataika mila na desturi tofauti. Mila na desturi uhusisha namna ya kuongea, mapishi, tofauti za ki-maendeleo baina ya kabila moja na nyingine. Si vizuri kuonyesha dharau hata kama ni katika hali ya utani kwa sababu hiyo huonyesha hisia zako dhidi ya mwenzako hata kama utasema unamtania.


6.    Epuka utani unaoeleka kweli uhalisia kimaumbile.


Jitahidi kuepuka utani unaohusiana na maumbile kama vile watu wafupi au wanene wana kasoro 1,2,3 n.k. wakati ukijua kwamba mwenza wako nao ana maumbile kama hayo. Utani kama huo hufanya mtaniwa kujisikia vibaya na kuleta migogoro katika ndoa.


7.    Kushaurishwa katika mambo ya msingi ki-familia.


Kitabia kila binadamu anapenda kuthaminiwa katika mambo tofauti tofauti kama kazi zake, ushauri n.k. Katika mambo ya msingi ya maendeleo ya kifamilia kama vile ununuzi wa kitu cho chote cha kifamilia kama vile samani, na vitu vingine muhimu katika maisha yetu ya kila siku.


Ili kuendelea kupata makala hizi weka jina lako na barua pepe kwenye kisanduku kidogo mkono wa kulia. 


Saturday 31 March 2018

MIGOGORO KATIKA NDOA/MAHUSIANO


Kama nilivyoeleza kwenye makala yangu ya changamoto zinazosababishwa na wanadoa wenye mmojawapo ni mawasiliano(kutokuelewana). Hii ndio changamoto kubwa sana katika ndoa na ndio chanzo cha taraka nyingi kwa mujibu takwimu za kimataifa. Kwa bahati mbaya tarakwimu za hapa kwetu nimeshindwa kuzipata kwa njia ya vyanzo rasmi vya vinavyohusika na takwimu.

Kimsingi ni kwamba migogoro inayosababishwa na kutoelewana chanzo chake kinaweza kuwa ni mmoja wa wanadoa au wote wawili. Migogoro kikawaida ipo kwenye ndoa zote ila hutofautiana kwa kiwango. Ipo kwenye kila ndoa kutokana na sababu za malezi na tabia za asili za wanandoa. Na kawaida migogoro ukua kutokana na kukosa utayari wa kuitatua kwa wanandoa wenyewe ama kwa wote wawili au mmoja wao. Inapotokea hakuna utayari kwa wote wawili, ndoa haiwezi kudumu na kama ni kwa mmoja wao tu kuna asilimia fulani ndoa kuweza kudumu na kama wote wako tayari kutatua ndoa hii inakuwa na asilimia 100 kudumu.

Kama nilivyoongea kwenye makala tajwa hapo juu. Migogoro ya kutoelewana ipo inayotokana na mahitaji ya kawaida na ya kimwili. Leo tutaongelea migogoro inayotokana na mahitaji ya kawaida ya kimwili. Ninavyosema mahitaji ya kawaida nina maana mahitaji ya msingi ya binadamu kama vile chakula, mavazi na mahitaji mengine ambayo siyo msingi yaani; mahitaji ya kumpendezesha mwanandoa, kushaurishwa, kuthaminiwa n.k.

NAMNA YA KUPAMBANA NA MIGOGORO INAYOTOKANA NA MAHITAJI YA KAWAIDA

1.    Kuwa mkweli kuhusu hali ya kipato chake.

Kuwa mkweli wa hali yako ki-uchumi yaani; kuwa mkweli kwa mwenza wako kuhusu hali ya mapato yako. Na ukweli huu ni vizuri ufanyike kabla ya kufunga ndoa. Ni vizuri sana kama utauvaa uhalisia wako kipato kipindi chote cha uchumba. Hili, ni muhimu sana kwa sababu nitakusaidia kujua kama mchumba wako ni wa kiwango chako au la. Ukidanganya katika suala hili unakuwa umepande mgogoro ambayo itakuwa vigumu kuusuluhisha na unakuwa umejenga hali ya kutoaminika.

2.    Onyesha kujali hitaji la mwenza wako.

Jitahidi kujali mahitaji ya mwenza wako kwa kumtimizia hitaji lake kama uwezo unaruhusu na kama unaona sihitaji la msingi, tafuta lugha nzuri ya kumweleza ni kwa nini unaona hitaji lisitimizwe na bila kuonyesha dalili za kupuuza au kuonyesha sihitaji la msingi.

3.    Epuka kuonyesha upendeleo katika kusaidia ndugu.

Katika familia zetu za ki-afrika kuna matatizo ya kila namna kwenye familia zetu yaani; kwa upande wa mke na mwanaume. Inapotokea kuna mahitaji upande wa familia za upande mmojawapo ni muhimu sana kuweka uwiano wa misaada inayotolea, ili kuepuka kuonyesha upendeleo.

4.    Epuka kuonyesha upendeleo kwa wageni wanao watembelea nyumbani.

Ni jambo la kawaida sana ndugu wa pande zote kutamani kuwatembelea wanandoa katika hali ya amani au matatizo. Ni vizuri kujitahidi kutoonyesha unyanyapaa kwa wanandugu wa upande mmoja hali hii inaweza kuleta mgogoro mkuu.

5.    Epuka kuonyesha dharau dhidi ya mila na desturi za mwenza wako.

Inapotokea wanandoa ni makabila tofauti ina maana watakuwa wamekulia kataika mila na desturi tofauti. Mila na desturi uhusisha namna ya kuongea, mapishi, tofauti za ki-maendeleo baina ya kabila moja na nyingine. Si vizuri kuonyesha dharau hata kama ni katika hali ya utani kwa sababu hiyo huonyesha hisia zako dhidi ya mwenzako hata kama utasema unamtania.

6.    Epuka utani unaoeleka kweli uhalisia kimaumbile.

Jitahidi kuepuka utani unaohusiana na maumbile kama vile watu wafupi au wanene wana kasoro 1,2,3 n.k. wakati ukijua kwamba mwenza wako nao ana maumbile kama hayo. Utani kama huo hufanya mtaniwa kujisikia vibaya na kuleta migogoro katika ndoa.

7.    Kushaurishwa katika mambo ya msingi ki-familia.

Kitabia kila binadamu anapenda kuthaminiwa katika mambo tofauti tofauti kama kazi zake, ushauri n.k. Katika mambo ya msingi ya maendeleo ya kifamilia kama vile ununuzi wa kitu cho chote cha kifamilia kama vile samani, na vitu vingine muhimu katika maisha yetu ya kila siku.

Ili kuendelea kupata makala hizi weka jina lako na barua pepe kwenye kisanduku kidogo mkono wa kulia. 




Wednesday 21 February 2018

FAIDA ZA KUSAMEHE

1. Kwanza kabisa, tunasamehe kwa sababu kusamehe ni amri na ni agizo la Mungu. binadamu ni watu ambao hawapendi kukubali kosa ni watu waliozoea kujitetea na kukataa kosa pale anapokosa. Kama tukikataa kutii tunakaidi agizo la Mungu hivyo tunapaswa kusameheana kwani muasisi wa msamaha ni Mungu mwenyewe na kama Mungu angehesabu maovu yetu nani angesimama? Anza leo kusamehe, hakuna aliye mkamilifu.
2. Tunasamehe ili tuweze kusamehewa na pia ili maombi yetu yaweze kupokelewa na Mwenyezi Mungu. Unapaswa kusamehe kwa faida yako mwenyewe siyo kwa faida ya mkosaji na mwachie Mungu apambane na watesi wako wala usilipe kisasi wewe mwekee mtesi wako kaa la moto kichwani limchome. Kumwekea kaa la moto kichwani ni kama kumtesa kisakikolojia wewe unamsamehe yeye, amini basi nafsi yake inaendelea kumtafuna.
3. Unasamehe ili uwe na Amani ya moyoni mwako. Unaposamehe unakuwa unapata amani ya moyo. Mtu ambaye anavumilia uchungu ulioumbika ndani ya moyo na hataki kuachilia fundo hilo lazima litamtesa na atakosa amani ya moyo. Atahangaika na huku uchungu ulioumbika ndani ya moyo ukiendelea kumtafuta.
4. Unasamehe ili uwe na furaha moyoni mwako. Kwa kweli ukiangalia watu wanaokataa kusameheana huwa hawana furaha kabisa katika mioyo yao. Kama unaishi katika mahusiano yoyote na mara nyingi huwa watu si wakamilifu basi msamaha ndio kiunganishi chenu ambao utarudisha uhusiano uliopotea au uliovunjika na kuleta uhusiano wa awali yaani uhusiano mpya.

5. Tunasamhe ili tuwe na afya njema. Uponyaji wa kweli unaanzia moyoni. Kama mtu anasamehe kutoka moyoni basi huo ni msamaha wa kweli na ni msamaha unaongozwa na huruma ya Mungu ndani yake. Watu hawataki kusamehe ndio maana wengine afya zao ni dhaifu. Uchungu ulioumbika ndani ya moyo unaendelaa kumtafuna. Usizeeke kabla ya wakati kwa ajili ya kutosamhe.
6. Kutosamhe kunakufanya ujikinai wewe mwenyewe. Unajiona wewe ni mtu ambaye hustahili kuwepo hapa duniani. Utajiona wewe hauna maana hapa duniani utakua unakaa peke yako peke yako. Huna furaha, amani, upendo. Maisha yako yanakuwa yamejaa sumu na majeraha moyoni ugonjwa umekuwa mkubwa na wewe hutaki kuupatia dawa ya kuuponya na dawa yake ni msamaha tu.
7. Kutokusamhe kunaongeza maadui katika maisha yako. Kuna faida kubwa sana ya kusamehe. Jaribu kuangalia katika maisha yako Yule anayesamehe na asiyesamehe nani anakuwa anaongeza maadui? Utaongeza maadui na utavunja uhusiano na watu hivyo utakua unaishi maisha ya umimi. Maisha ya binadamu ni maisha yenye uhusiano kama husamehi basi unajitengenezea duniani yako mwenyewe.
8. Kutosamhe kunaleta mapasuko wa kifamilia. Katika hali ya kawaida jaribu kuangalia katika jamii yako ni familia ngapi zimesambaratika kwasababu ya kutosameheana ? ni nyingi sana kwanza familia nyingi zina migogoro ya aina mbalimbali inayosababishwa na watu kulipiana visasi na kutosameheana na kuishi maisha ya chuki kama ya paka na panya. Kusamehe ni faida kwa kila familia bora inayotaka amani na furaha, mipasuko katika familia itaendela kuwepo kama watu wasiposameheana.
9. Kutosamhe kunaleta unyonge wa moyo yaani huzuni. Ukiwaangalia watu wengine unawaonea huruma wanaishi maisha ya huzuni wakati falsafa ya maisha ni furaha hapa duniani. Tunatafuta kila siku ili tuweze kuwa na furaha. Inuka leo na nenda kazike hilo jeneza la huzuni na kuwa huru na maisha yako. Huoni ni utumwa kuwabeba watu moyoni? Hujaja duniani kuteseka na maisha ni mafupi sana samehe na endelea na maisha yako.
10. Kutosamhe kunawafanya watu kukimbia makazi na ofisi zao. Kwa mfano, watu waliokoseana na hawataki kusameheana huwa wanaishi maisha kama ya paka na panya. Akimuona mwenzake huyo anakuja anakimbia kama yuko nyumbani anakimbia, kama ni njia anabadilisha kabisa ili wasionane na kusalimiana. Unakuta watu wengine wanakimbia kabisa ofisi zao kwa sababu ya kutotaka kusameheana. Kwanini uendelea kuishi maisha haya? Anza kubadilika kama ulikuwa unakimbia makazi au ofisi ili usikutane na mtesi wako.

Maisha ya kutokusamehe yanahasara nyingi na faida ni nyingi zaidi kuliko hasara. Imani za watu zinakufa kwa ajili ya kutokusamehe, watu wanazeeka mapema kabla ya muda, watoto wa mitaani wanaongezeka kwa ajili ya kutokusamehe yaani; pale wazazi wanapotalakiana na kuwatelekeza watoto. Tuishi katika maisha ya kusameheana na siyo ya kulipizana visasi.


Kwa ushauri tuwasiliane kwa barua-pepe fkmwamoto@gmail.com au Whatsapp 0784190882