Saturday 30 April 2016
Friday 29 April 2016
MAMBO SITA (6) YANAYOWATIA HOFU WANAWAKE KATIKA NDOA
Karibu
ndugu wasomaji wa wavuti hii, leo napenda kuongelea mambo sita yanayowatia hofu
wanawake kwa waume zao pamoja ustawi wa ndoa zao. Kutokana na tafiti mbalimbali
na uzoefu wa kimazingira kuna hofu nyingi wanazokuwa nazo wanawake dhidi ya
waume zao hasa kwa ndoa changa na ambazo hazikupitia hatua ya uchumba wa muda
mrefu. Kama iliyohada mke na mme hukutana wakiwa wote ni watu wazima
waliyokulia katika mazingira, utamaduni na familia tofauti wakapendana na
kufikia maamuzi ya hiari ya kufunga ndoa. Kutokana na mzingira, makuzi,
utamaduni, mtazamo n.k. watu wanapokuwa wameamua kufunga ndoa hutokea hofu za
kimahusiano za hapa na pale ambazo kila mmoja hujitahidi kuziondoa. Tafiti za
kisaikolojia zinasema hujengwa katika mtazamo hasi. Baadhi ya hofu hizo ni kama
zifuatazo: -
©
Hofu
ya kutoridhishwa katika tendo la ndoa.
©
Hofu
ya kutomridhisha mmewe katika tendo la ndoa.
©
Hofu
ya mmewe kupotea hamu ya ndoa.
©
Hofu
ya mmewe kumkinai na kuanza michepuko.
©
Hofu
ya mmewe kutobadilika katika baadhi ya matendo yasiyompendeza.
©
Hofu
ya kutokua kiroho kama wanandoa.
Naomba
nifafanue kidogo juu ya hofu hizo sita hapo juu.
©
Hofu ya kutoridhishwa katika tendo
la ndoa na mmewe.
Kutokana
tafiti na ushahidi wa kimazingira ndoa nyingi zinazofungwa sasa zinakutanisha
wanandoa wenye uzoefu wa viwango tofauti wa tendo la ndoa ambao wameupata kwa
wanaume wengine tofauti na mme anayefunga nae ndoa. Hii inatokana na jamii
kukosa maadili ya ki-utamaduni na kidini upande wa malezi.
Wanawake
wengi wanaingia katika ndoa kwa kufuata hali ya uchumi ya muoaji au kutokana na
umri kuwatupa mkono na hivyo kujiingiza katika ndoa na shinikizo hizo mbili,
kwa sababu wenye kukidhi haja za tendo la ndoa hawahitaji kuwaoa au ni waume wa
watu. Kutokana na uzoefu wa kukutana na wanaume mbalimbali na wengi kutokidhi
haja zao za tendo la ndoa huingia katika ndoa na hofu hii. Tafiti zinaonyesha
kwamba mwanamke akitembea na wanaume kumi ni mmoja au sifuri wenye uwezo
wakumridhisha katika tendo la ndoa. Na hii ndio inayowafanya kuingia katika
ndoa na hofu hiyo, licha ya kwamba asilimia kubwa ya ndoa za siku hizi wanandoa
wengi huingia kwenye ndoa wakiwa wanajuana vizuri. Lakini huingia kwenye ndoa
kwa kutegemea kwamba wenza wao
watabadilika na kuweza kuwaridhisha kadri watakavyoendelea kuishi.
©
Hofu ya kutomridhisha mmewe katika
tendo la ndoa.
Kama
nilivyongea kwenye kipengele cha hapo juu ya uzoefu wa kufanya tendo la ndoa
kabla ya ndoa. Pamoja na uzoefu wa kuachwa na wanaume mbalimbali zikiambatana
na kashfa mbalimbali kutoka kwa wanaume waliyowaacha huwajengea hofu ya kukidhi
haja ya waume zao ya tendo la ndoa. Na kwa wanandoa ambao hawaongelei kabisa
juu ya tendo hilo na hawana maandalizi kabla na tendo la ndoa huishi katika
hofu hiyo maisha yao yote.
Hii ni changamoto
kubwa sana katika ndoa nyingi dunia nzima, ndio talaka zinazidi kuongezeka.
©
Hofu ya mmewe kupoteza nidhamu ya
ndoa.
Kawaida
ukiwa katika ndoa kuna nidhamu ambayo lazima izikatiwe kama vile muda wa kurudi
nyumbani, matumizi, ulaji nakadhalika kwa ndoa ambazo wanandoa wanaheshimiana.
Katika ndoa ambayo wanandoa wanheshimiana kila mmoja ni mlinzi wa mwenzie yaani
kuagana na kujulishana kila mmoja alipo inakuwa ni jambo la kawaida kabisa.
Kutokana na
ndoa nyingi kupoteza nidhamu mme kulala nje, kuchelewa kurudi nyumbani n.k. wanawake
wengi huwa na hofu ya ndoa zao kuingia katika misukosuko ya aina hii.
©
Hofu ya mmewe kumkinai na kuanza
michepuko.
Kutokana na
hofu ya kutokumridhisha mmewe hofu ya kukinaiwa na mmewe hujitokeza.
©
Hofu ya mmewe kutobadilika katika
baadhi ya matendo yasiyompendeza.
Kutokana na sababu ya kuingia kwenye
ndoa kutokana shinikizo nilizozitaja hapo juu, wanandoa wengi hugundua kwamba
wenzio wao mara nyingine wanatabia ambazo ni kero kama vile ubishi, uchelewaji
kurudi nyumbani bila taarifa, kufanya mambo ya msingi bila kumshirikisha
mwenza, kutopenda kula nyumbani n.k. Mambo haya kimsingi huleta msongo wa
mawazo pale ambapo mme anaambia kujirekebisha lakini anakuwa mgumu kubadilika
kwa sababu ya tabia za mfumo dume.
©
Hofu ya kutokua kiroho kama
wanandoa.
Katika nchi hasa za ki-afrika kuna
ndoa za aina tatu(3):
ü Kiserikali
ü Kimila
Tafiti zinaonyesha kwamba ndoa
nyingi zinafungwa kidini, kutokana na hofu nilizozitaja hapo juu suluhisho
pekee linategemea imani ya wahusika. Hili kutatua matatizo hayo hapo hali ya
imani ya kidini ya wanandoa ni muhimu sana kwa maana taasisi hii mwanzilishi ni
Mungu mwenyewe kwa mujibu vitabu vya kidini. Kwa hiyo, Imani inapokuwa chini ni
vigumu sana kutatua hofu zinazojitokeza katika taasisi hii muhimu sana.
Nimeongea kifupi kwenye kila
kipengele na ninaamini kila jambo linasuluhisho katika dunia hii. Naomba nipate
maoni yenu.
Thursday 28 April 2016
UMUHIMU WA KUWA NA FAMILIA BORA ILI KUJENGA JAMII BORA.
Habari mpenzi msomaji wa wavuti hii? Na karibu katika makala yetu
ya leo ambapo leo tutajifunza umuhimu wa kuwa na familia bora ili kujenga jamii
bora. Bila familia bora hakuna jamii bora ambayo italeta maendeleo katika
dunia. Tunapenda kujifunza mambo ya familia au tunasoma mambo ya familia kwa
sababu kuu mbili;
Kwanza, sisi sote tumezaliwa katika familia. Hakuna mtu hapa duniani ambaye hajazaliwa katika familia ndio maana sisi sote tumezaliwa katika familia na tunapaswa kujifunza sana mambo ya familia.
Pili, familia ni msingi wa maisha ya mtu. Kila mtu anapata msingi wa maisha kutoka katika familia yake. Baba na mama wakimpatia mtoto msingi mzuri wa maisha yake basi mtoto atakwenda kujenga jamii iliyo bora kabisa. Ndio maana watu wako tofauti sana hii ni kutokana na kila mtu amepata msingi wa maisha tofauti na kuna wengine wamepata msingi mzuri wengine wamepata msingi mbaya.
Kwanza, sisi sote tumezaliwa katika familia. Hakuna mtu hapa duniani ambaye hajazaliwa katika familia ndio maana sisi sote tumezaliwa katika familia na tunapaswa kujifunza sana mambo ya familia.
Pili, familia ni msingi wa maisha ya mtu. Kila mtu anapata msingi wa maisha kutoka katika familia yake. Baba na mama wakimpatia mtoto msingi mzuri wa maisha yake basi mtoto atakwenda kujenga jamii iliyo bora kabisa. Ndio maana watu wako tofauti sana hii ni kutokana na kila mtu amepata msingi wa maisha tofauti na kuna wengine wamepata msingi mzuri wengine wamepata msingi mbaya.
Kwa kawaida familia inajengwa na baba, mama na watoto au mtoto. Familia ni kiungo cha msingi katika jamii. Mungu amepanga kila mtu kuzaliwa katika familia. Mtoto anajenga maadili na mtazamo wake kuhusu yeye mwenyewe, ulimwengu na maisha kutoka katika familia kulingana na mazingira alipozaliwa na alipokulia.
Ili tujenge jamii bora tunatakiwa kwanza tujenge familia bora kwa sababu kila mtu ametokea katika familia. Ndani ya familia baba na mama wanapaswa kuwafundisha watoto maadili mema tokea wakiwa wadogo kuwa mafunzo ya jinsi kuishi, kuwa na maadili mazuri. Mtoto akikosa kupewa upendo katika familia na kufundishwa falsafa hii kubwa ya upendo atakwenda kutengeneza jamii mbovu kama mtoto anatoka katika familia ambayo baba na mama wanaishi maisha ya uadui, ugomvi yaani kama vile maisha ya chui na swala. Mtoto anaona baba na mama wanapigana tokea akiwa mdogo je unafikiri anajenga nini katika akili yake? Baba ni mlevi wa kupindukia, wazazi wote wawili wanakosa upendo, hawaheshimiani wanatukanana mbele ya watoto, nyumba haina amani kila mtu na mambo yake matokeo yake wazazi wanapandikiza chuki kwa watoto matokeo yake ni kujenga jamii mbovu.
Familia ikiishi katika falsafa ya upendo tutajenga jamii bora yenye upendo. Upendo wa kujipenda wewe mwenye na watu mwingine. Familia ikikosa kuishi katika msingi imara wa upendo wanakwenda kujenga jamii ambayo haina hofu na mtu ambaye hana hofu atafanya kitu chochote anachojisikia na kuleta madhara makubwa kwa jamii. Kutokua na upendo hakuna huruma ya Mungu watu wanatenda mambo ya ajabu ambayo chanzo chake ni kukosa msingi bora kutoka katika familia.
Familia inayowajibika katika kufanya kazi kwa bidii, kila mmoja kutekeleza wajibu wake bila shuruti itajenga jamii bora. Familia kuwafundisha watoto kuwajibika ni mafanikio ya familia kuongeza kizazi kingine bora ambacho ndio jamii. Bila familia hakuna jamii. Jamii inapata faida kupitia familia, jamii inapata watu wanaowajibika kutoka katika familia. Familia ni mali ya jamii. Familia ikiwa nzuri na jamii itakua nzuri. Hivyo basi, familia ikiharibika na jamii inaharibika.
Watoto wanaathirika sana kisaikolojia wakiangalia matendo mabaya kutoka kwa wazazi. Mwisho wa siku watoto wanawachukia wazazi kwa matendo yao , watoto wanakata tamaa ya maisha na kuona hakuna sababu ya kuishi je kama familia imejengwa kwa msingi kama huu tutatengeneza jamii iliyo bora?
Mtu anafahamika katika jamii kama mtu wa familia fulani. Mtoto wa familia fulani na mzaliwa wa sehemu fulani. Kwa hiyo, familia inakuwa chanzo cha kujenga maisha ya mtu na familia ni muhimu sana katika malezi.
Makala hii imeandikwa na Deogratius Kessy ambaye ni mwandishi, mhamasishaji na mjasiriamali, unaweza kuwasiliana naye kupitia namba 0717101505 au kwa barua pepe deokessy.dk@gmail.com au unaweza kutembelea tovuti yake www.actualizeyourdream.blogspot.com
Monday 25 April 2016
MCHAKATO WA KUPATA MCHUMBA mwendelezo
Habari za siku
nyingi ndugu zangu wasomaji wa wavuti hii. Samahani sana kwa ukimya wa muda
mrefu sana, kwa sababu ni siku nyingi sana nimeanza makala hii, naomba leo
niimalize kwa kuiongelea kwa kifupi ili tuendelea na makala zingine. Michakato
inayofuatia ni kama ifuatavyo: -
4. Kumshukuru Mungu
Ki-imani
tunaamini kwamba mke/mme mtu hupewa na Mungu hasa kama umemshirikisha/ulimuomba
kama mchakato unavyoeleza hapo juu. Na hii, ni kwamba kuoa/kuolewa ni mpango wa
Mungu wa kuongeza kizazi cha wanadamu.
5. Msichana/Mwanamke kuwajulisha wazazi
wake
Baada
ya kumshukuru Mungu na kuafikiana kwenda kuwajulisha wazazi juu ya azma ya kuwa
mke na mme hatua inayofuta ni msichana/mwanaume kwenda kuwajulisha wazazi juu
ya suala la kumpata mwenza.
6. Mvulana/mwanaume kwenda kwa wazazi
wa mwanamke kuchumbia
Hatua ya mwisho ni wazazi wa mvulana/mwanaume kwenda
kwa wazazi wa msichana/mwanaume kwenda kuchumbia ili hatimaye waweze kufunga
ndoa.
Naomba
nipate maoni yenu kuhusu makala husika.
Subscribe to:
Posts (Atom)