Saturday 22 November 2014

SIFA 14 ZA MWANAUME BORA ALIYEOA


Ahsante sana msomaji kwa kuamua kujiunga na Blogu hii awali ya yote napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu muumba wa mbingu na nchi kwa kunipatia uzima na ufahamu mpaka kuniwezesha kuandika machache kuhusu mada ya leo inayosomeka; sifa za mwanaume bora aliyeoa. Sifa husika ni kama zifuatazo: -
? Mcha Mungu.
? Anampenda mkewe.
? Anamheshimu mkewe.
? Mwaminifu katika ndoa.
? Ni msafi.
? Uwathamini ndugu wa mkewe sawa na ndugu zake.
? Anajua kumlinda/kumtunza mkewe na familia kwa ujumla.
? Mwenye bidii katika kazi.
? Asiwe mlevi wa kilevi aina yo yote.
? Asiwe mgomvi, mtukanaji, mtesaji, mtesi nakadhalika.
? Ni mfariji wa mkewe.
? Uomba ushauri kwa mkewe katika maamuzi muhimu ya kifamilia
? Usamehe na kuomba msamaha anapokosewa/anapokosea
? Ni huru kueleza hisia zake kwa mkewe.

Sifa hizo hapo juu pia ndio sifa bora kwa mchumba bora kwa kiume.
Ufafanuzi wa kina wa kila kipengele unapatikana kwenye blogu ya http://mkombozi-mahusiano.blogspot.com ambayo gharama yake ya kujiunga uwanachama ni TZS. 10,000.00 malipo yafanyike kwa Airtel Money  0784190882 au TiGO pesa 0719841988. Blogu hii imeshehena makala mbalimbali kuhusiana na mbinu za kujenga na kuboresha mahusiano. Fanya uamuzi hutajutia uamuzi wa kujiunga na blogu husika.

Karibu kwenye makala ijayo na waalike na wenzio, ili uendelee kupata maarifa ya kuimarisha na kuboresha mahusiano.

Monday 10 November 2014

MIHIMILI MIKUU Y A NDOA

Habari za majukumu mbalimbali ya kiuchumi ndugu wasomaji wa wavuti hii, bila shaka nyote ni wazima kwa uweza wa mwenyezi Mungu muumba mbingu na nchi. Kwa wale ambao afya zao zimetetereka kidogo Mungu yu pamoja nanyi mtapona.
Leo napenda kutaja mambo matano (5) muhimu ambayo ni mihimili mikuu inayofanya ndoa yo yote iweze kudumu: -
1)      Uvumilifu.
2)      Ucha Mungu.
3)      Bidii ya kazi.
4)      Roho ya kujitawala.
5)      Roho ya kusamehe.
Mihimili tajwa hapo juu imepangwa si kwa mfuatano wa kipaumbele bali imepangwa kiholela.
Ufafanuzi wa kina wa kila kipengele unapatikana kwenye blogu ya http://mkombozi-mahusiano.blogspot.com ambayo gharama yake ya kujiunga uwanachama ni TZS. 10,000.00 malipo yafanyike kwa Airtel Money  0784190882 au TiGO pesa 0719841988. Blogu hii imeshehena makala mbalimbali kuhusiana na mbinu za kujenga na kuboresha mahusiano. Fanya uamuzi hutajutia uamuzi wa kujiunga na blogu husika.

Karibu kwenye makala ijayo na waalike na wenzio, ili uendelee kupata maarifa ya kuimarisha na kuboresha mahusiano.

Monday 20 October 2014

JIPATIE MCHUMBA UNAYEMPENDA

Kutokana na maoni na ushauri wa wasomaji wengi, nimekubali kutengeneza Blogu mpya  http://jipatiemchumba.blogspot.com itakayowaunganisha watu mbalimbali kuwa wapenzi kwa lengo la kufunga ndoa kwa mapenzi ya Mungu.

Ili kuweza kupata kibali cha kuingia kwenye blogu tajwa hapo juu ni budi:-
1)      Tuma  TZS. 5,000.00 kwenye 0719841988 au blockchain bitcoin address nitakayokupatia kwa baruapepe yangu.r
2)      Tuma  anuani pepe (E-mail address) yako ya google kwa fkmwamoto@gmail.com pamoja na kumbukumbu namba ya pesa uliyotuma. Kama huna anuani pepe ya google nakushauri ufungue au uombe msaada kwangu.
3)      Toa sifa zako kwa mtiririko ufuatao: -
                                        i.            Umri wako:
                                      ii.            Jinsia:
                                     iii.            Kimo cha chako:
                                    iv.            Rangi yako:
                                      v.            Kazi yako:
                                    vi.            Elimu yako:
                                   vii.            Tabia usiyoipenda: ......................(e.g. Ulevi, Uvutaji sigara, n.k)
                                 viii.            Dini yako:
                                    ix.            Unapenda nini? …………………………(e.g. Muziki, kujisomea, kuangalia TV n.k)   
Ambatanisho picha yako pasipoti au kamili. Kamili ni vizuri zaidi)
4)      Unayemtaka awe na sifa zifuatazo:-

                                             i.            Umri wake:
                                           ii.            Jinsia:
                                          iii.            Kimo chake:
                                         iv.            Rangi yake:
                                           v.            Kazi yake:
                                         vi.            Elimu yake:
                                        vii.            Tabia usiyopendezwa nayo:
                                      viii.            Dini yake:
                                         ix.            Awe anapenda kitu gani?

5)      Uanachama kwenye Blogu hii, utasitishwa kwa mwanachama ye yote iwepo:-

                                             i.            Iwapo mwanachama atabainika kumtukana mwanachama mwenzie kwa njia ya sms/e-mail kwa sababu ya kushindwa kuafikiana.
                                           ii.            Atasambaza namba ya simu/anuani pepe ya mwanachama mwenzake pasipo idhini ya husika.
Vigezo vitaendelea kuongezeka kadiri hali itakavyotulazimisha kufanya, karibu usikate tamaa mme/mke utaweza kumpata kwa kupitia blogu hii.



Friday 29 August 2014

NGUZO KUMI ZA MAHUSIANO

Habari za majukumu mbalimbali ya kiuchumi ndugu wasomaji wa blogu hii, bila shaka nyote ni wazima kwa uweza wa mwenyezi Mungu muumba mbingu na nchi. Kwa wale ambao afya zao zimetetereka kidogo Mungu yu pamoja nanyi mtapona.
Leo napenda kutaja mambo kumi muhimu katika kudumisha mahusiano ya aina yote lakini hasa ndoa na uchumba: -
1.       Mungu.
2.       Upendo.
3.       Roho.
4.       Kujitolea
5.       Agano.
6.       Kukubaliana.
7.       Mawasiliano.
8.       Kusameheana.
9.       Kujitawala.
10.   Kuwa msaada kwa mwenza wako.

Ufafanuzi wa kina wa kila kipengele unapatikana kwenye blogu ya http://mkombozi-mahusiano.blogspot.com ambayo gharama yake ya kujiunga uwanachama ni TZS. 10,000.00 kwa Airtel Money  0784190882 au TiGO pesa 0719841988. Blogu hii imeshehena makala mbalimbali kuhusiana na mbinu za kujenga na kuboresha mahusiano. Fanya uamuzi hutajutia uamuzi wa kujiunga na blogu husika.

Karibu kwenye makala ijayo na waalike na wenzio, ili uendelee kupata maarifa ya kuimalisha na kuboresha mahusiano.


Tuesday 12 August 2014

LENGO LA NDOA

Habari za majukumu mbalimbali ya kiuchumi ndugu wasomaji wa blogu hii, bila shaka nyote ni wazima kwa uweza wa mwenyezi Mungu muumba mbingu na nchi. Kwa wale ambao afya zao zimetetereka kidogo Mungu yu pamoja nanyi mtapona.
Leo napenda kuongelea malengo la ndoa kwa muktadha wa Mungu ambaye ndie muasisi wa ndoa katika bustani ya Eden. Kwa lengo makala hii, ndoa ninayoiongelea hapa ni ya watu wa jinsi tofauti yaani; mwanamke na mwanaume. Sababu za msingi za kuweka ndoa ni kama zifuatazo: -
Ø  Kuondoa upweke.
Ø  Kusaidiana kupambana na changamoto za kimaisha.
Ø  Kujenga familia.
Ø  Kuendeleza kizazi.
Ø  Kukidhi tamaa ya mwili.
Ø  Kuakisi upendo wa Mungu.
Sababu hizo sita (6) ninaweza kuzifafanua ifuatavyo: -
Kuondoka upweke; Kama nilivyoongea kwenye utangulizi Mungu ndie mwanzilishi wa taasisi hii ya ndoa katika Bustani ya Eden. Binadamu wa kwanza kuumbwa Dunia alikuwa ni Adam baada ya kuona yu mpweke Mungu alimuumba Hawa kuwa msaidizi wake kutoka kwenye ubavu wa Adam.
Kusaidiana kupambana na changamoto za kimaisha;Maisha yanachangamoto nyingi sana za kiuchumi, kiafya, ki-imani nakadhalika ukipata mke au mme ambae ni chaguo sahihi/bora atakusaidia kupambana na changamoto za kimaisha. Mke na mme sahihi hupatikana kwa msaada wa mwenyezi Mungu. Kwenye makala ya namna ya kupata mchumba kuna maelezo ya kujitosheleza kuhusu mada hii. Makala hii, inapatikana kwenye blogu yangu ya http://mkombozi-mahusiano.blogspot.com ambayo utaratibu wake wakujiunga nitawafahamisha hapo mbele.
Kujenga familia; Familia ni baba, mama na mtoto/watoto. Ni dhahiri kwamba mke na mme kwa majaliwa ya mwenyezi Mungu wakifahamiana kimwili matokeo yake ni mimba hatimaye mtoto au watoto kutegemea na watakavyokuwa wanaamua wao wenyewe. Kwa hiyo kujenga familia ni mmojawapo wa lengo la kufunga ndoa japo kwa baadhi ya watu mtoto au watoto si lengo lao!
Kuendeleza kizazi; Kusudi la mwenyezi Mungu kuweka mbegu kwa viumbe vyote hai wakiwemo na binadamu ni ili kuendeleza kizazi cha uumbaji wake. Kila kiumbe kiliumbwa na mbegu ya kukiendeleza yaani; mmea, wanyama pamoja na binadamu, ndege wa angani, viumbe wa majini nakadhalika.
Kukidhi tamaa ya mwili;Binadamu aliyepevuka ameumbwa na tamaa ya kufanya tendo la ndoa. Ndoa imeweka na mwenyezi Mungu kuwa ni unganiko halali la kukidhi tamaa ya mwili ya tendo la ndoa kwa wanandoa.
Kuakisi upendo wa Mungu; Mungu ni pendo na hii ndio sifa kuu ya Mungu ambayo anapendo wanadamu wawe nayo. Ndoa uunganisha mme na mke kuwa mwili mmoja kimwili, kihisia, ki-imani vyote hivi vikiwa vimejengwa katika msingi wa upendo. Mme na mke wataachana na wazazi wao na kuungana kuwa mwili mmoja kwa sababu ya kupendana.
Mkabidhini Mungu awe kiongozi wa maisha ya ndoa yenu siku zote kwa maana yeye ndie muasisi ya taasisi ya ndoa,  hakika ndoa yenu itadumu na itakuwa kisima cha amani na furaha na kielelezo cha mfano kwa ndoa nyingine. Na pia nakushauri ujiunga na blogu ya http://mkombozi-mahusiano.blogspot.com kwa TZS. 10,000.00 kupitia huduma ya Tigo na  Airtel Money  kupitia  0719841988 na 0784190882 upate makala zenye maarifa tele ya masuala ya mahusiano na ushauri.
Jiunge na blogu tajwa hapo UPATE MAARIFA YA KUPUNGUZA MIGOGORO KATIKA MAHUSIANO, TUJENGE TAIFA IMARA. Pia nakaribisha maoni yako kuhusu makala za blogu hii.

Wednesday 30 July 2014

MATARAJIO YA WANANDOA KWENYE MAISHA YA NDOA

Wanandoa huwa na matarajio mengi sana katika maisha yao ya ndoa hasa matarajio mazuri daima.  Maisha ya ndoa ni mchakato ambao hupita katika hatua kuu nne (4) yaani; kuzaliwa, kukua, kuzeeka na kufa. Lakini si ndoa zote hupitia hatua hizo zote nne (4) baadhi hupitia hatua tatu (3) au mbili (2) kutokana na baadhi ya wanandoa kuacha kumkabidhi mlezi na mwanzilishi wa ndoa duniani yaani; Mungu. Kwenye makala hii, sitaki kuongelea sababu anuai zinazosababisha baadhi ya ndoa kutopitia hatua kuu nne (4) mzunguko wa maisha ya ndoa. Baadhi ya matarajio maisha ya iliyo katika hatua ya pili (2) ni kama yafuatavyo:-
ü  Changamoto za masuala ya kifedha.
ü  Changamoto za kimawasiliano baina yao.
ü  Changamoto zinazoletwa na wanandugu na watoto.
ü  Upweke.
ü  Kukua/kudumaa kiroho.
ü  Migogoro.
ü  Magonjwa.
Kipengere cha 4 hadi 7 nitavifafanua lakini cha 1 hadi 3 zilishavifanunua kwenye makala zangu za awali za changangamoto zinazosababishwa na wanandoa wenyewe na changamoto zinazosababishwa watu wengine wasiyowanandoa.
Upweke; Kutokana na kuongezeka kwa majukumu na uwajibikaji kwa masuala ya kifamilia maisha uliyokuwa unategemea kuwa yatakuwa daima ya amani na furaha huanza kubadilika na hapo ndipo hali ya kutaka kukaa kiupweke uanza kujitokeza ili kutafari zaidi majukumu ya kifamilia na hamu ya tendo la ndoa hupungua kwa sababu ubongo unakuwa umezingirwa na mawazo ya namna ya kutatua majukumu yaliyo mbele kama vile ada, kodi ya nyumba, gharama za usafiri kwenda na kurudi kazini, chakula nakadhalika.
Migogoro; Kutokana ndoa kuwa katika hatua ya kukua  tabia zote zilizokuwa zimevichwa na wanandoa wote uanza kudhihirika kwa sababu tabia haiwezi kufichwa daima. Tabia za kiburi, jeuri, dharau, hasira, uasherati nakadhalika uanza kuonekana na kuleta migogoro ya hapo pale katika ndoa. Hatua hii inahitaji busara na hekima kubwa hasa kwa kumshirikisha Mungu, ili kuweza kuivuka na ndoa nyingi sana huishia hatua hii.
Magonjwa; Kwa sababu za kimazingira na vyakula imekuwa ni jambo la kawaida kwa binadamu kuugua kwa muda mrefu au mfupi. Inapotokea uuguaji ni wa muda mrefu jambo ili uyumbisha sana hali ya uchumi wa wanandoa na kama hakuna upendo wa dhati basi hata misingi ya ndoa uanza kulegalega.
Mwacheni Mungu awe mtawala katika maisha yenu ya ndoa kwa maana yeye ndie muasisi ya taasisi ya ndoa hakika ndoa yenu itadumu na itakuwa kisima cha amani na furaha. Na pia nakushauri ujiunga na blogu ya http://mkombozi-mahusiano.blogspot.com kwa TZS. 10,000.00 kupitia huduma ya Tigo na  Aairtel Money  kupitia  0719841988 na 0784190882 upate makala zenye maarifa tele ya masuala ya mahusiano.
Jiunge na blogu tajwa hapo UPATE MAARIFA YA KUPUNGUZA MIGOGORO KATIKA MAHUSIANO, TUJENGE TAIFA IMARA.





Monday 21 July 2014

NYENZO ZA KUSTAWISHA NDOA

Napenda kuchukua nafasi hii, kwanza kumshukuru Mwenyezi Mungu muumba wa mbingu na nchi kwa kunipa nafasi hii adimu ya kuwaandikieni makala hii fupi. Pia napenda kuchukua nafasi hii kuwashukuru wasomaji  wangu wapendwa wa mabara yote kwa kuendelea kunitia moyo kwa ushauri na maoni yenu mazuri,  nawaombeni muwaalike na marafiki zenu kusoma makala za blogu hii.
Kwa tafsiri isiyo rasmi nyenzo ni kifaa cha kufanyia kazi. Kwa musktadha wa makala hii nyenzo imetumika kwa maana ya kanuni. Napenda kutajwa nyenzo za kustawisha ndoa kwamba ni kama zifuatavyo: -

a)    Kubali kuwa wewe ndio chanzo cha mgogoro
b)    Kutokata tamaa (tumaini)
c)     Kusamahe
d)    Beba hisia za mwenzako (Empathy)
e)     Kujitoa
Ufafanuzi wa nyenzo hizo ni kama ifuatavyo: -
Kubali kuwa wewe ndio chanzo cha mgogoro; Ni kawaida ya wanandoa kusukumia lawama kwa ndugu, jamaa, marafiki  na watoto kuwa ndio chanzo cha migogoro katika ndoa. Jambo ili si sahihi kwa sababu ndugu, jamaa, marafiki na watoto ni matokeo ya ni nyi kuwa mwili mmoja yaani; kufunga ndoa. Migogoro yo yote inayojitokeza katika ndoa chanzo chake ni wanandoa wenyewe; ndugu, jamaa, marafiki na watoto wao ni wachocheze tu ili kukoleza moto ili uweka zaidi. Hapa nina maana kwamba chanzo cha kutoa siri au kasoro zo zote zilizomo ndani ya ndoa ni wanandoa wenyewe. Kwa hiyo, wanandoa kama watakuwa radhi kuongelea na kuzitafutia suluhu changamoto zao za kwenye ndoa kisirisiri wanakuwa na asilimia mia moja ya kustawisha ndoa yao bila shaka yo yote.
Kutokata tamaa; Maisha yamejaa changamoto nyingi sana na changamoto hizi zipo kwa ajili ya kukufanya uweze kufikia mafanikio yaani; ni daraja kuelekea kwenye mafanikio. Changamoto katika ndoa zipo nyingi sana na nyingi huletwa na wasiliano mabovu baina ya wanandoa wenyewe (Kwa uelewa zaidi juu ya hili bofya hapa), hali ya uchumi, ndugu, jamaa, marafiki nakadhalika. Jambo kubwa hapa ni kuwa na matumaini ya suluhu na kuitafuta dhidi ya changamoto zo zote zinazojitokeza kwa sababu hakuna changamoto isiyo kuwa na njia ya utatuzi.
Kuwa tayari kusamehe; Kusamehe ni agizo la Mungu na pia ni ishara ya busara. Mme/mke si malaika kwa hiyo yeye kufanya makosa ni jambo la kawaida la kibinadamu. Jitahidi kusamahe kadri uwezevyo na muelimishe mwenzako kadri uwezevyo mpaka ufike mahali pa kumuelewa vema. Ili zoezi mnatakiwa mlifanye maisha yenu yote ya ndoa kwa sababu makosa mengi hufanywa pasipo kukusudia.
Beba hisia za mwenzako (Empathy); Jitahidi kumuelewa mwenzako na beba hisia zake. Kwa kufanya hivyo, itakuwa rahisi sana kudumisha ndoa yenu kwa maana haitakuwa rahisi kumfanyia ukatili au kumlazimisha kufanya jambo ambalo wewe mwenyewe usingependa kufanyiwa. Yaani hisia za upendo na huruma zitatawala maisha yenu daima.
Kujitoa; Changamoto za ndoa ni nyingi sana na ili ndoa iweze kudumu inahitaji wanandoa wote kwa pamoja wawe na moyo wa kutojitoa kwa lengo la kuhakikisha kwamba ndoa yao inadumu, bila hivyo ndoa nyingi zisingekuwa zinadumu. Ninaposema kutojitoa nina maana kuwa radhi kukubaliana na mambo hata yasiyokupendeza ili mradi tu ndoa yao iwe endelevu. Vipengere vyote hapo juu (a mpaka d) vinawezekana tu iwapo kutakuwa na moyo wa kujitoa.
Mweke Mungu mbele katika maisha yenu ya ndoa kwa maana yeye ndie muasisi ya taasisi ya ndoa hakika ndoa yenu itadumu na itakuwa kisima cha amani na furaha. Na pia nakushauri ujiunga na blogu ya http://mkombozi-mahusiano.blogspot.com kwa TZS. 10,000.00 kupitia huduma ya Tigo na  Aairtel Money  kupitia  0719841988 na 0784190882 upate makala zenye maarifa tele ya masuala ya mahusiano.
Jiunge na blogu tajwa hapo UPATE MAARIFA YA KUPUNGUZA MIGOGORO KATIKA MAHUSIANO, TUJENGE TAIFA IMARA.


Tuesday 15 July 2014

MALEZI YA WATOTO

Napenda kuchukua nafasi hii kwanza kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa nafasi hii adimu ya kuwaandikieni makala hii fupi. Pia napenda kuchukua nafasi hii kuwashukuru wasomaji  wangu wapendwa kwa kuendelea kunitia moyo kwa ushauri na maoni yenu mazuri, naomba muendelee na moyo huo na nawaombeni muwaalike na marafiki zenu kusoma makala za blogu hii.
Leo naomba niongelee jukumu la malezi ya watoto ni la nani? Je, ni la Baba, Mama, Baba na Mama, Walimu, Viongozi wa dini au ni la jamii. Watoto ni zao la ndoa yaani; ni matokeo ya msichana/mwanamke na mvulana/mwanaume walioamua kuungana kama mke na mme. Japo kutokana na kukosekana kwa maadili katika jamii kuna watoto wanapatikana nje ya ndoa.
Baba; Katika jamii za kiafrika na jamii zingine pia mwanaume ndio kichwa cha nyumba. Na mara nyingi uwajibika kwa kuhakikisha mahitaji yo yote ya nyumbani yaani; chakula, mavazi na malazi yanapatikana. Lakini inapotokea mtoto kafanya makosa kazi ya kumuadibisha mtoto linaleta ugomvi miongoni mwa wazazi hao yaani; utasikia mama akigomba kwa kusema muache mtoto wangu hujui nilivyoteseka “labor” nakadhalika. Hili si sawa hata kidogo. Kwa sababu lengo ni kumweka sawa mtoto kimaadili.
Mama; Katika jamii za ki-afrika mwanamke/mama ubeba jukumu la malezi ya watoto kuanzia mimba mpaka mtoto.Malezi ya mama hujikita kwenye masuala ya kuhakikisha wamekula, wanavaa nguo safi, wanalala mahali pazuri nakadhalika. Lakini hujiepusha sana na kuadhibu watoto wanapokosea na jukumu hilo kulipeleka kwa baba lakini kwa tahadhari kubwa. Nimetumia neno tahadhari kwa maana kwamba mtoto inapotokea kaadhibiwa huwa tena wa kwanza kuomba asiadhibiwa sana na baba na hivyo kuonekana wanamapenzi na urafiki sana ya watoto kuliko baba. Lakini tabia hii si kwa akina mama wote. Baadhi ya akina mama ni kubeba jukumu la malezi kikamilifu yaani; uchukua jukumu la kuadhibu watoto inapobidi bila kusita badala ya kumpa baba jukumu hilo.
Baba na Mama; Jukumu la baba na mama ni kuhakikisha watoto wanaandaliwa mahitaji yote muhimu ya kimaisha ya kila siku aidha na yeye mwenyewe au kwa kumtumia mfanyakazi wa nyumbani. Pia na kuhakikisha kwamba watoto wanalelewa katika maadili yanayokubalika kifamilia na kijamii. Hii ni pamoja na kuhakikisha kwamba watoto wanapata elimu bora na maadili ya kidini kwa mujibu wa imani yao au ya mmoja wao.
Walimu; Wanachukua nafasi muhimu sana katika malezi ya watoto kuanzia elimu ya chekechea hadi chuo kikuu. Hawa wana nafasi muhimu sana katika kuhakikisha kwamba wanamuandaa mtoto kwa maisha ya kujitegemea kwa kumpatie utaalamu wa kumuwezesha kuendesha maisha yake kwa manufaa yake na taifa kwa ujumla. Lakini wazazi pia wanatakiwa kuwasaidia walimu kuhakikisha kwamba yale wanayofundishwa watoto wana yazingatiwa na yanaeleweka na watoto.
Kwa bahati mbaya baadhi ya walimu siku hizi wamekengeuka na wanaonekana kuchangia katika kuharibu watoto wakiume na wakike kwa kutembea nao. Yaani; baadhi ya walimu wakike na wanatembea na wanafunzi wakiume na walimu wakiume wanatembea na wanafunzi wakike.
Viongozi wa dini; Wanachukua sehemu muhimu ya kuwajenga watoto ki-imani kutegemea na imani ya wazazi wao kwa Mungu wanaomwamini.
Lakini kwa bahati mbaya baadhi ya viongozi wa dini wamekuwa wakifanya kinyume na haya mpaka kufikia hatua ya kutembea na watoto wa waumini wao. Hili si sawa hata kidogo linahitaji kukemewa na jamii.
Jamii; Jamii inawajibu mkubwa sana katika malezi ya watoto kwa sababu watoto ni zao la jamii. Lakini kutokana na jamii kukengeuka jambo hili aliko sawa na linavyotakiwa kuwa. Katika jamii ya leo, hakuna mzazi anayepata ujasiri wa kumuonya/kumuadhibu mtoto asiye wake kwa sababu ya kuogopa kutukanwa na mtoto au kuchukuliwa hatua na mzazi wake.
Katika jamii ya leo sio ajabu kuona mama au baba mtu mzima akitembea na mtoto wa jirani yake au wa kwake. Hili si sawa hata kidogo linahitaji kukemewa na jamii.
Mshirikisheni Mungu katika malezi ya watoto wenu kwa sababu ni tunu mliyopewa kwa kusudi maalumu. Na pia nakushauri ujiunga na blogu ya http://mkombozi-mahusiano.blogspot.com kwa TZS. 10,000.00 kupitia huduma ya Tigo na  Aairtel Money  kupitia  0719841988 na 0784190882 upate makala zenye maarifa tele ya masuala ya mahusiano.
Jiunge na blogu tajwa hapo UPATE MAARIFA YA KUPUNGUZA MIGOGORO KATIKA MAHUSIANO, TUJENGE TAIFA.IMARA.






Monday 7 July 2014

CHANGAMOTO ZA KUPATA MCHUMBA KATIKA JAMII

Habari za leo ndugu wasomaji wa blogu hii. Nina imani nyote kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu muumba wa mbingu na nchi hamjambo na ni wazima wa afya na kama kuna ambaye afya yake si njema Mwenyezi Mungu atanijalia atapona muda si mrefu.
Siku ya leo nitaongelea changamoto za kupata mchumba katika kipindi hiki cha maendeleo makubwa ya Sayansi na Teknolojia. Uchumba ni mahusiano baina ya mwanaume na mwanamke kwa lengo la kufunga ndoa na kuwa mke na mme baada ya kila mmoja kuridhika na mwenzake. Katika makala ya utambulisho wa blogu hii kuna maelezo yenye kujitosheleza zaidi kuhusiana na neno hili.
Kwa siku za hivi karibuni kuna malalamiko ya kila upande yaani; wanaume na wanawake kuhusiana na suala la uchumba kwa kwamba wanaume hawataki kuoa na wanawanake hawataki kuolewa.  La kujiuliza tatizo ni nini hapo?  Kimsingi sababu zipo nyingi  sana na baadhi ni kama zifuatavyo : -
1)   Tabia.
2)   Tamaa.
3)   Kukosekana kwa sifa alizoziweka.
4)   Kukosekana kwa maadili katika jamii.
Ufafanuzi wa sababu hizo hapo juu na ni vipi zinachangia changamoto za kupata mchumba na hatimaye ndoa ni kama ufuatavyo:
Tabia; Ni kipengere muhimu sana kinachoangaliwa wakati wa utafuta wa mchumba yupi anafaa katika jamii. Msichana/mvulana mwenye tabia nzuri jamii inayomzunguka ndio inayomnadi msichana/mvulana mwenye tabia inayokubalika katika jamii. Yaani; “ule usemi wa kizuri cha jiuza na kibaya cha jitembeza” ujidhihilisha bayana katika hili. Kwa maana hiyo, suala la kupata mchumba kwa msichana/mvulana mwenye tabia inayokubalika katika jamii kunakuwa hakuna shida hata kidogo kwa maana kina mtu utamani kuwa mchumba wa msichana/mvulana husika. Kwa bahati mbaya hili uwahusu sana wasichana kwa kwa sababu wao ndio wanaoombwa uchumba na wanaume.
Tamaa; Kuna tabia inayoendelea kujengeka siku hadi siku ya mali kuwa ni kigezo cha kukubaliwa kuwa mchumba wa mtoto wa familia fulani au la.  Sasa katika familia binti anapomwambia mzazi wake kwamba nimepata mchumba swali la kwanza analoulizwa mtoto ni anafanya kazi gani, au ana mali gani badala ya kuuliza kama wanampendana au la. Na ikibainika kwamba anayetafuta uchumba kwa binti hana kitu hiyo inakuwa ni sababu ya kukataliwa kuwa mchumba wa binti yao.  Kutokana na sababu hiyo mabinti wengi sana wamezuiliwa kuwa wachumba wa wanaume waliyowapenda kwa dhati ya mioyo yao.  Kwa jamii za zamani mtoto anaposema amepata mchumba suala la kwanza lililokuwa linafanywa na wazazi ni kuanza kuchunguza ukoo husika una magonjwa gani ya kurithi, ukoo huo una taswira gani katika jamii nakadhalika.
Kukosekana kwa sifa alizoziweka; Kuna tabia iliyojengeka kwa baadhi ya wanawake na wanaume kupanga vigezo vya mme/mke anayetaka kuwa mchumba wake ambavyo mara nyingi ina kuwa ni vigumu sana kuvifikia vyote.  Vigezo/Sifa kama vile mrefu, mwembamba, maziwa makubwa/madogo, tabia nzuri, elimu ya kiwango fulani nakadhalika. Kimsingi ni kwamba huwezi kupata sifa zote hizo kwa mtu mmoja ni vigumu sana. Katika harakati ya kutafuta mchumba mwenye sifa hizo zote mara nyingi hujikuta wakikosa kupata mchumba kwa wakati muafaka na hatimaye kuamua kuolewa/kuoa mtu ambaye hawaendani na hana sifa hata moja kati ya hizo. Hivyo kujikuta wakiwa kwenye ndoa bila kuwa na furaha wala amani moyoni wao baada ya kuona wakati hauko upande wake.
Kukosekana kwa maadili katika jamii; Kutokana na kukosekana kwa maadili wanawake na wanaume wengi hufanya vitendo visivyo na maadili katika jamii kama vile ufuska, ulevi, nakadhalika na kuona suala la kuwa na mchumba si la lazima. Hii ni kwa sababu unapovunjika unaleta hasara na lawana nyingi na hata kifo/vifo kwa wahusika
Mshirikishe Mungu katika mipango ya maisha yako yote kwa maana yeye ndiye mwenye mpango mkakati wa maisha yako hapo duniani.  Na pia nakushauri kujiunga na blogu ya http://mkombozi-mahusiano.blogspot.com kwa TZS. 10,000.00 kupitia huduma ya Tigo na  Aairtel Money  kupitia  0719841988 na 0784190882 upate makala zenye maarifa makini ya masuala ya mahusiano.
Jiunge na blogu tajwa hapo UPATE MAARIFA YA KUPUNGUZA MIGOGORO KATIKA MAHUSIANO, TUJENGE TAIFA.IMARA.