Wednesday 28 May 2014

MAMBO 4 YANAYOATHIRI MAKUZI YA WATOTO

Katika hali inayokubali katika jamii zetu, mtoto ni matokeo ya wawili waliyokubaliana kuishi kama mke na mme baada ya kufunga ndoa. Japo mara nyingine watoto wanapatikana nje ya ndoa. Leo niongee mambo manne (4) yanayoathiri makuzi ya mtoto kwa ujumla.
Makuzi ya mtoto/watoto ni jukumu la muhimu sana kwa mzazi yo yote katika jamii.

Katika tafiti mbalimbali za kisayansi makuzi anayopata mtoto kuanzia umri wa miaka 0 hadi 12 yanaakisi tabia atakayokuwa nayo katika utu uzima wake. Mambo 4 yafuatayo yanaathiri makuzi ya mtoto ni kama yafuatavyo: -
1. Kuadibisha: Hatua za kinidhamu unazochukua kwa mtoto wako huathiri malezi yake. Wataalam wa malezi ya watoto wanashauri malezi yetu yawe shirikishi kwa maana ya kwamba kila unapomkataza mtoto kufanya jambo fulani kama vile kutukana watu, utoro shuleni, ugomvi n.k ni vizuri zaidi ukawa unamfahamisha ni kwa nini haifai kufanya jambo fulani, ili kumpatie nafasi ya kuhoji/kutafakari/kuelewa badala ya kumshurutisha tu kutekeleza maagizo.  Kwa kufanya hivyo, unampa uwezo wa kupambanua, kuelewa na kujiamini katika maamuzi mbalimbali. Pia hatua kali za kinidhamu kama vile kumchapa mtoto zinaweza kusababisha hofu kwa watoto wako, ambayo huathiri uwezo wao wa kuwasiliana na wewe, walimu hata wenzao pia.  Hata hivyo, pia kuwa mpole mno wanaweza kuendeleza ukosefu wa nidhamu na kuathiri mwenendo wa mtoto katika jamii na shule.
2. Mazingira: Neno mazingira kwa tafsiri fupi ni vitu vyote vinavyotuzunguka hewa, miti, majengo, watu, wanyama, shule, nyumba za ibada .n.k. Mazingira ya mtoto yanaathiri ya moja kwa moja kwa mtoto hasa ya nyumbani na shuleni. Muda mwingi wa makuzi ya watoto hutumika nyumbani na shuleni. Mtoto anayetoka kwenye nyumba ambayo wazazi wake wako katika hali ya ugomvi kila mara, umasikini, utajiri n.k. mambo hayo uathiri moja kwa moja utazamo wa mtoto wa kimaisha. Pia mtoto ambaye anasoma shule ambayo kila saa anakosa amani kutokana na kutishiwa kupigwa na walimu au wanafunzi wenzie hujengewa hali ya kuwa na wasiwasi na kutopenda kwenda shuleni na shule.
3. Mawasiliano: Mtoto ashirikishwe katika baadhi ya maamuzi ya ki-familia kama vile masuala ya chakula, vinywaji, maongezi n.k. Ninaposema kushirikishwa katika suala ya chakula ni katika hali ya kujenga tabia ya ushirikishwaji na kumpa uhuru wa maamuzi kumuuliza mtoto leo unataka kula nini mama/baba ni kuonyesha kuthamini mawazo yake. Pia katika maongezi nina maana mtoto sema jambo lo lote ni muhimu kumsikiliza na siyo vizuri kumpuuza au kumkaripia kwamba anapiga kelele. Tabia hiyo, itamsaidia kwa kumpatie uwezo wa kujieleza na kujisikia kuthaminiwa na wazazi wake.
4. Malezi:  Mfumo wako wa malezi unaweza kumjenga mtoto wako au kuharibu. Kuweka ratiba ya kukaa na watoto na kuongea nao na kusikiliza mawazo hayo huwajengea hali ya kujisikia kuathaminiwa na kupendwa na wazazi/walezi na hivyo  kuwaongezea furaha na amani. Pia tabia hii huwajengea hali ya kujiamini na uhuru wa kueleza hisia zao nyumbani na shuleni bila hofu kwa sababu ya Imani ya kupendwa imejengwe kwenye akili zao.
Kwa hiyo, wazazi tuna jukumu kubwa sana katika kujenga watoto wetu kisaikologia katika umri wa miaka 0 hadi miaka 12. Kumjenga mtoto baada ya miaka 12 na kuendelea inakuwa vigumu sana, japo inaweza kumbadilisha.
Jiunge na blogu ya http://mkombozi-mahusiano.blogspot.com ili UPATE MAARIFA YA KUPUNGUZA MIGOGORO YA MAHUSIANO, TUJENGE TAIFA.IMARA. Maoni na ushauri mbalimbali yanakaribishwa. Karibu PAMOJA TUSONGE MBELE.


Saturday 24 May 2014

TARATIBU ZA KUWA MWANACHAMA WA BLOGU MPYA

Kutokana na maoni na ushauri wa wasomaji wengi, nimekubali kutengeneza Blogu mpya  http://jipatiemchumba.blogspot.com itakayowaunganisha watu mbalimbali kuwa wapenzi kwa lengo la kufunga ndoa kwa mapenzi ya Mungu.
Ili kuweza kupata kibali cha kuingia kwenye blogu tajwa hapo juu ni budi:-
1)      Tuma  TZS. 10,000.00 kwenye 0719841988 kwa Tigo pesa.
2)      Tuma  anuani pepe (E-mail address) yako ya google kwa fkmwamoto@gmail.com pamoja na kumbukumbu namba ya pesa uliyotuma. Kama huna anuani pepe ya google nakushauri ufungue au uombe msaada kwangu.
3)      Toa sifa zako kwa mtiririko ufuatao: -

                                        i.            Umri wako:
                                      ii.            Jinsia:
                                     iii.            Kimo cha chako:
                                    iv.            Rangi yako:
                                      v.            Kazi yako:
                                    vi.            Elimu yako:
                                   vii.            Tabia usiyoipenda: ......................(e.g. Ulevi, Uvutaji sigara, n.k)
                                 viii.            Dini yako:
                                    ix.            Unapenda nini? …………………………(e.g. Muziki, kujisomea, kuangalia TV n.k)   
Ambatanisho picha yako pasipoti au kamili.
4)      Unayemtaka awe na sifa zifuatazo:-

                                             i.            Umri wake:
                                           ii.            Jinsia:
                                          iii.            Kimo chake:
                                         iv.            Rangi yake:
                                           v.            Kazi yake:
                                         vi.            Elimu yake:
                                        vii.            Tabia usiyopendezwa nayo:
                                      viii.            Dini yake:
                                         ix.            Awe anapenda kitu gani?

5)      Uanachama kwenye Blogu hii, utasitishwa kwa mwanachama ye yote iwepo:-

                                             i.            Iwepo mwanachama atabainika kumtukana mwanachama mwenzie kwa njia ya sms/e-mail kwa sababu ya kushindwa kuafikiana.
                                           ii.            Atasambaza namba ya simu/anuani pepe ya mwanachama mwenzake pasipo idhini ya husika.
Vigezo vitaendelea kuongezeka kadiri hali itakavyotulazimisha kufanya, karibu usikate tamaa mme/mke utaweza kumpata kwa kupitia blogu hii.


CHANGAMOTO ZA MAHUSIANO ZINAZOLETWA NA WATU WENGINE WASIYOWANANDOA

Napenda kuwashukuru wale wote walionitumia ujumbe kwa ushauri na maoni. Leo nitazungumzia changamoto zinazosababishwa na watu wengine wasio wanandoa kama nilivyosema kwenye makala ya utambulisho wa blogu hii. Kwa sababu wanandoa wanaishi katika jamii, ndugu wa karibu na marafiki. Hawa wanajamii, ndugu wa karibu na marafiki wanakuwa ni chanzo cha changamoto nyingi katika ndoa kutokana na wanandoa kutokuwa na msingi imara wa ndoa yao.
Baadhi ya sababu zinazosababisha changamoto katika ndoa na watu wengine wasiyo wanandoa ni kama zifuatazo: -
Watoto: Watoto ni mibaraka katika ndoa, lakini mara nyingine huleta migogoro katika ndoa kutokana na kutoelewana wanadoa kuhusu  kuwaadabisha watoto wao na mambo mengine ya msingi kwa ajili ya watoto. Katika suala la kuwaadabisha watoto mara nyingi hutokea mmoja ya mzazi kumgombeza mwenza inapotokea mtoto anaadhibiwa na mmoja wa wazazi kwa sababu ya wawili hao kutokuwa na msimamo mmoja kuhusiana na malezi ya watoto wao. Na suala hili husababisha watoto kujenga chuki kwa mzazi anayewaadisha na upendo kwa yule anayewatetea.
Ndugu wa wanandoa: Mara nyingi hutokea wanandugu kama vile mawifi, mashemeji, wakwe nakadhalika kuwa na sauti sana kwenye masuala ya ndoa ya ndugu yao. Mambo yanayosababisha migogoro kutoka kwa wanandugu ni hutegemezi  kwa mmoja wa wanadoa. Mara nyingi ndugu hutaka kuendelea kuwaongoza wanandoa kuhusu suala la matumizi ya pesa na kusahau kwamba masuala hayo inatakiwa yaongozwe na wanandoa wenyewe kwa kuzingatia vipaumbele vyao. Hii huleta migogoro sana kwa sababu wanandugu kutotaka kutambua ushrikikishwaji wa mkewe/mmewe katika suala la misaada pande zote mbili za kwa mkewe/mmewe na kwao pia.
Kazi: Kutokana na kutumia muda mwingi sana kazini mara nyingi wanandoa wengi hujikuta wakiwa hawana muda wa kuongea na kupanga mipango muhimu ya kimaendeleo,  malezi ya watoto wao na mambo ya unyumba pia. Kutokana kutingwa na kazi nyingi wanandoa wengi hujikuta wakimaliza shida zao nje ya ndoa na kushindwa kutimiza majukumu yao ya msingi kiunyumba nyumbani kwa visingizio mbalimbali.
Marafiki: Kutokana na kukosa misingi imara, ndoa nyingi zinaangukia mikono mwa marafiki kutokana na wanandoa wenyewe kukosa maadili na kutoa siri za ndoa kwa marafiki. Hii, hutokea kwa lengo la kuomba ushauri kwa marafiki zao ambao mara nyingi huwa si marafiki wema, uwazunguka na kuwasaliti na hata kupinduka ndoa za marafiki wao.
Watumishi wa nyumbani: Mara nyingi kutokana na kukosa umakini katika masuala muhimu ya kinyumba ndoa nyingi hujikuta zikiyumbishwa na watumishi wa nyumbani wa kiume na wakike kutokana na wanandoa wengi kukosa umakini, uaminifu na tamaa za ngono. Umakini hukosekana kwa kumpa mtumishi majukumu wengi yasiyostahili kupewa mtumishi kama vile usafi wa chumbani, kutandika kitanda  nakadhalika.
Mali: Mara nyingi mali husababisha ndoa nyingi  kudumu pasipo uimara wo wote  kwa mmoja wa wanandoa kuwa mtumwa wa mali za mmoja wa wanandoa. Mara nyingi mali husababisha wanandoa wengi kuwa na tamaa ya kutoka sana nje ya ndoa kwa sababu kwa kutumia mali hiyo wanakuwa na uwezo wa kumnunua mwanamke/mwanaume yo yote na kufanya nae ngono  na hivyo kusababisha ndoa kukosa heshima. Mara nyingine kuna wanandoa wanaingia kwenye ndoa na watu wenye mali kwa lengo la kuchota mali kwa njia ya kudai taraka muda mfupi baada ya ndoa kwa visingizio mbalimbali kwa kwenda mahakamani kudai taraka ambao kisheria mali iliyochumwa kipindi cha ndoa hugawanywa kati yao.
Ili kupata maarifa ya kukabiliana na migogoro mbalimbali inayojitokeza katika taassis hii, kuwa mwanachana wa blogu ya http://mkombozi-mahusiano.blogspot.com ambayo huingiaji wake ni kwa kuzingatia taratibu zilizoelezwa kwa kwenye makala zangu zilizotangulia.
Jiunge na blogu tajwa hapo UPATE MAARIFA YA KUPUNGUZA MIGOGORO KATIKA MAHUSIANO, TUJENGE TAIFA.IMARA.


Monday 19 May 2014

CHANGAMOTO ZINAZOSABABISHWA NA WANANDOA WENYEWE SEHEMU YA 2

Katika makala ya kwanza tulijadili jinsi kutoelewana/mawasiliano kwa wanandoa wenyewe kunavyosababisha changamoto/migogoro katika ndoa. Leo tutajadili jinsi Usaliti, Udanganyifu, Uchoyo, Kukosa maadili, Uchafu na kufichana taarifa za muhimu (Kabla na ndani ya ndoa), nakadhalika.
Usaliti: Katika mtazamo wa kindoa ni kitendo cha mwanandoa kutoka nje ya ndoa yaani; kufanya uasherati. Sababu kubwa za usaliti ni tamaa ya kimwili na ngono, kutoelewana katika ndoa, ulevi, ugonjwa wa muda mrefu wa mmoja wa wanandoa, marafiki n.k.
Katika sababu zote tajwa hapo juu inayotawala sana katika kusababisha usaliti ni tamaa ya kimwili na ngono. Yaani; kutokana na tamaa ya vitu ambayo mara nyingi wanandoa hawana uwezo wa kuvilimiki vitu fulani kwa mfano; nguo za thamani, vito vya thamani, kujipendezesha, chakula n.k mara nyingi hujikuta wakiingia katika usaliti kwa lengo la kujipatia kipato, ili kukidhi tamaa za kimwili. Usaliti wa kingono unatokana ya tabia au mapungufu kimahusiano ya kindoa ambayo sababu zake kutoelewana kimwili. Kubaliana na mgogoro huu ufafanuzi wake upo kwemye makala ya blogu nitakayoitaja hapa chini.
Ulevi ni moja ya sababu ya wanandoa wengi kutoka nje ya ndoa kwa sababu ulevi hupunguza utashi wa maamuzi kwa baadhi ya watu.
Marafiki mara nyingine hushawishi baadhi ya wanandoa wasiyokuwa na misimamo kutoka nje ya ndoa kwa tamaa ya mahitaji ya kimwili.
Udanganyifu: Ni tabia ya kutokuwa mkweli katika kauli na vitendo. Tabia hii, si tabia ya asili ni tabia inayotokana na malezi. Tabia hii, katika ndoa si nzuri kwa sababu udanganyifu husababisha wanandoa kutoamini.
Uchoyo: Ni tabia ya kutopenda kutoa. Tabia hii, inatokana na malezi. Tabia hii, husababisha wanandoa mara nyingi kutengwa na wanandugu na marafiki na jamii inayowazunguku.
Kukosa maadili: Maadili ni tabia zinazokubalika katika jamii. Yaani; mambo yanayokubalika katika jamii kama vile kuheshimiana kwa rika, lugha isiyo ya matusi. Kwa kifupi ni utii wa mila na desturi. Tabia hii ya kukosa maadili ni zao la malezi. Kwa hiyo, kukosa maadili ni kwennda kinyume na mila na desturi za jamii kama vile kutokuheshimu wakwe, mme, tabia za matusi, dharau za wazi n.k.
Uchafu: Ni tabia ya kutopenda usafi. Tabia hii, inaweza kuwa ya asili au ikitokana na malezi. Tabia hii, inaleta sana migogoro katika ndoa nyingi bila kujali tabia hii, iko kwa mwanaume au mwanamke. Tabia ni mbaya sana kwa sababu ni rahisi kupata magonjwa kwa wanandoa na watoto.
Kufichana taarifa muhimu ( kabla na ndani ya ndoa): Taarifa muhimu ambazo wanandoa wanapaswa kujulishana kabla ya ndoa ni kama vile; magonjwa ya kiukoo miongoni mwa wanandoa, uzazi wa kabla ya ndoa, n.k. Taarifa muhimu kupeana ndani ya ndoa ni kipato, majukumu yo yote nje ya yale ya wanandoa, mipango ya kimaendeleo kama vile ujenzi wa nyumba n.k. Kipengere hiki, kina changamoto nyingi ambazo mbinu za kuzikabili zimefafanuliwa zaidi kwenye makala inayopatikana kwenye Blogu yangu nyingine inayoitwa http://mkombozi-mahusiano.blogspot.com ambayo wenye uwezo wa kuingia ni wale tu ambayo wametimiza masharti ya Blogu husika. Masharti yako ni kutuma TZS. 10,000.00 kwenye 0784190882 airtel money na baada yapo nitumie anuani pepe yako ya google, kama una ni vizuri ukafungua.
Visababishi vyote hivyo hapo juu, vinaweza kuepukika iwepo wanandoa wenyewe wataamua/ watadhamiria kufanya hivyo. Madhara yatokanayo na changamoto katika ndoa yametajwa kwa makala yangu ya utambulisho wa blogu, ili kuiona makala hiyo bofya kwenye maandishi ya bluu.
Jiunge na blogu tajwa hapo UPATE MAARIFA YA KUPUNGUZA MIGOGORO KATIKA MAHUSIANO, TUJENGE TAIFA.IMARA.

Tuesday 13 May 2014

CHANGAMOTO ZINAZOSABABISHWA NA WANANDOA WENYEWE

Kama nilivyosema kwenye Utambulisho wa Blogu hii, kwamba makala yangu hii, itaongelea sababu za changamoto/migogoro inazosababishwa na wanandoa wenyewe.
Kabla sijaongelea changamoto zinazobabishwa na wanandoa wenyewe. Ni vizuri nikaongelea mahusiano yalipo kati ya ndoa na taifa yaani; mchango wa ndoa katika kujenga taifa na tabia za watu katika taifa lo lote. Ndoa ni chanzo cha taifa lo lote kuwa lilivyo hivi sasa yaani; kuwa na nguvu au dhaifu. Kama tujuavyo taifa hujengwa na hubolewa na watu wake, kwa sababu ndio wanaokuwa  viongozi, watunga sera, wakulima, wataalamu na wafanyakazi wakuu wa kila sekta wa taifa husika. Kama tujuavyo misingi ya tabia ya binadamu yo yote inaanza kujengwa/kubomolewa akiwa bado tumboni mwa mamaye na hatimaye akiwa mtoto mchanga chini ya baba na mama, mama pekee, baba pekee kutegemea na mazingira  Mungu aliyompanga mtoto huyu alilelewe. Mtoto hujengwa au hubomolewa vipi? Kimalezi akiwa tumbo ni somo refu sana, lakini kwa sababu si lengo la makala hii kufundisha somo hilo sitaliongelea. Mtoto akishazaliwa, walezi wake wakuu wanakuwa ni baba na mama, mama pekee, baba pekee, mtaa  pamoja na jamii inayomzunguka, huanza kufundisha mila na desturi za jamii husika. Ukilelewa katika familia ya wacha Mungu, wachapa kazi, wavuvi, waongo, watukanaji, wagovi na wewe utajifunza tabia hizo. Kimsingi kila binadamu huwa na mafungu mawili ya tabia yaani; tabia ya kujifunza na ya asili (kuzaliwa na nazo). Lakini hapo napenda kuongelea tabia zinazotokana na mazingira au za kufundishwa na zinaathiri vipi, maisha katika ndoa.
Kwa hiyo, mimi/wewe tabia nilivyo/ulivyo ni  matokeo ya malezi niliyopata/uliyoyapata katika makuzi yangu/yako nikiwa/ukiwa chini walezi wako pamoja na tabia ya asili yaani; yakuzaliwa nayo.
Ni vizuri pia, msomaji wangu ungefahamu kwamba familia huzaa jamii na jamii huzaa taifa.. Kwa tafsiri fupi isiyo rasmi; ndoa ni zao la familia, familia nyingi huitwa jamii na jamii nyingi ndio huunda taifa. Ndoa ni muunganiko wa hiari wa mtoto wa familia moja na nyingine wa jinsia tofauti kuwa mke na mme. Hapa neno mtoto limetumika kwa maana ya zao la familia si kwa maana ya umri. Ki-umri kila nchi ina sheria yake kuhusiana na umri unaofaa kwa msichana kuolewa. Kwa hiyo, ndoa ni muunganisha wa watu wawili waliolelewa katika malezi tofauti.
Changamoto za kwenye ndoa zinazosababishwa na wanandoa wenyewe chanzo chake kinaanzia kwenye malezi waliopata wanandoa husika katika makuzi yao. Malezi huzaa tabia na tabia kuna inayoletwa na mazingira na ya asili. Tabia ni somo kubwa ambalo linahitaji makala maalum.  Visababishi vya changamoto zinazotokana na wanandoa wenye ni matokeo ya tabia zao wenyewe wanandoa. Baadhi ya sababu hizo ni mawasiliano(kutoelewana), usaliti, udanganyifu, uchoyo, kukosa na maadili, n.k  na katika makala hii nitajadili changamoto ya mawasiliano.
MAWASILIANO (KUTOELEWANA)
Sababu hii ni chanzo kikubwa cha changamoto/migogoro mingi sana katika jamii nyingi sana katika dunia yetu hii.
Changamoto hii, kiini chake ni mmojawapo wa wanandoa au wote wawili kutotaka kumsikiliza mwenza mahitaji/mawazo yake iwe ya vitu au ya kimwili kwa ukaidi au kutokuwa na uwezo wa kutimiza au kutokuwa tayari kumsikiliza mwenza mantiki yake katika hitaji husika. Kwa lugha nyingine changamoto  hii ninaweza kusema ni kutoelewana.
Katika hali ya kawaida ukiona watu wawili ni marafiki sana ujue mmoja au wote wako tayari kusikiliza wazo la mwenzie kwa umakini na kulikubali au kulikata na kueleza sababu za kulikataa kwa kujenga hoja za kumshawishi sababu za kutokukubaliana nae pasipo kumuudhi mtoa wazo. Kusikiliza kwa makini nina maana huonyesha kihisia kwamba unajali hitaji lake. Kuonyesha kujali umfanya kujiona unanthamini kwa kiasi kikubwa na kumuondolea unyonge.
Hivyo hivyo pia,  katika ndoa ni muhimu sana kuheshimu hitaji la mwenzi wako na kulifanyia kazi. Kuliheshimu hitaji la mwenzi wako hakumaanisha kulikubali tu hata kama sio nzuri hapana, ila kama hukubaliani nalo toa sababu za msingi ni kwa nini hukubaliani na wazo husika na kutoa mawazo yako mbadala pasipo kuonyesha kupuuza/kudharau mawazo yake.
Kutimiziana mahitaji ya kimwili ni jambo moja la msingi katika ndoa. Lakini kikubwa hapa ni kwamba unalitimizaje? Ili, kuweza kuondoa malalamiko kwenye suala hili, kujuana ni jambo la muhimu sana. Na hili linawezeka kama wawili hawa  wakiwa  wazi katika hitaji hili. Hii inasaidia kujua namna ya kumuridhisha kila husika katika hitaji husika pasipo kumletea shida au kuleta malalamiko kutoka kwa mmojawapo wao. Ninaposema shida nina maana inatakiwa kila mmoja ajue njia muafaka ya kumridhisha  mwenzie. Kimsingi akina mama mara nyingi ni wa wanga wa kutoridhishwa na wenzi wao kwa sababu ya kutokuwa wa wazi au wenzie wao kuwa na ubinafsi zaidi kwa kutaka kuwatumia wenzi wao kama “Robot”. Robot ni chombo kinachotengenezwa na binadamu chenye uwezo wa kufanyishwa kazi kama binadamu kwa mfano; kufanyakazi viwandani, mashambani, kuongoza magari n.k.
Nisingependa kuwachosha kwa kuandika makala ndefu sana, visababishi vingine vya changamoto za ndoa vinavyosababishwa na wandoa wenyewe nitaendelea navyo kwenye makala itakayofuata.
Kwa ushauri kuhusiana na changamoto za ndoa na uchumba tuma jambo lo lote unalohitaji ushauri  kwenye anuani pepe fkmwamoto@gmail.com na utajibiwa kupitia anuani pepe yako.
Hili kuweza kuingia kwenye blogu yenye makala za ushauri mbalimbali wa migogoro ya mahusiano,  tuma shilingi elfu kumi tu (TZS. 10,000/=) kwenye airtel money 0784190882. Halafu nitumie anuani pepe yako na jina la usajili la laini uliyotumia kutuma pesa kwenye anuani pepe hapo juu. Hii ni ada ya kukuwezesha kuingia na  kusoma makala za Blogu hiyo, utapata maarifa/mbinu za kukabiliana changamoto za mahusiano, hivyo kujiepusha na magonjwa yaletwayo na changamoto hizo kama vile Shinikizo la damu, kisukari, UKIMWI n,k. Karibu TUJENGE TAIFA IMARA.

Sunday 11 May 2014

UTAMBULISHO WA BLOGU

Kabla sijaeleza madhumuni ya blogu hii ningependa kutoka tafsiri  isiyo rasmi ya maneno makuu katika jina la Blogu hii yaani; Ushauri, Changamoto, Ndoa na Uchumba.

Ushauri ni mawazo mapya kutoka mtu/taasisi yo yote ambayo muombaji wa huduma hiyo anaamini kwamba itampatia mawazo mazuri ya kumfanya asonge mbele dhidi ya changamoto zinayokukabili. Na lengo la ushauri ni kupata mawazo mbadala au njia ya kuepukana/kukabiliana na changamoto au mzigo wa muathirika. Mara nyingi ushauri umfanya mshauriwa kupata faraja na imani na kujisika katika hali ya kawaida kimawazo na kupata nguvu mpya.
Changamoto ni jambo lo lote lililo mbele yako ambalo linakusumbua na unaliona ni kikwazo katika mustakadhali wa maisha yako, hivyo kuhitaji msaada dhidi jambo husika kutoka kwa mtu/ taasisi unayemwamini/unayoiamini. Changamoto mara nyingi uletwa na mabadiliko ya kimazingira au watu wanakuzunguka hii ni tafsiri fupi, kwa hapo mbele tutapata tafsiri nyingi na rasmi. Kihistoria changamoto katika ndoa zilianzia katika Bustani ya Eden baada ya Hawa kukaidi maagizo ya Mungu aliyoambiwa na mmewe Adam ya kutokula tunda la mti wa katikati ya Bustani ya Eden.
Ndoa ni muunganiko wa hiari baina ya mwanaume/mvulana na mwanamke/msichana kuwa mme na mke kwa lengo la kuunda familia. Muunganiko huu ni kawaida urasmishwa ki-dini, kiserikali na ki-mila. Kihistoria ndoa ya kwanza katika dunia hii, ilikuwa baina ya binadamu wa kwanza katika sayari yaani; Adam na Hawa katika Bustani ya Eden. Lengo kuu ikiwa ni kumuondolea upweke Adam katika Bustani ya Eden kwa Mungu kuamua kumpatia anayefananaye.
Uchumba ni mahusiano ya karibu sana baina ya mwanaume/msichana na mwanamke/msichana ambao unafahamika na wazazi wa pande zote kwa lengo la kufunga ndoa kwa maridhiano ya wawili hao.
MADHUMUNI YA KUUNDWA KWA BLOGU HII
Madhumuni ya blogu hii ni kutoa ushauri wa kitaalamu wa namna sahihi ya kukabiliana na changamoto zinazojitoka kila kukicha katika tasnia hizi za ndoa na uchumba katika sayari yetu hii dunia. Ushauri wa namna ya kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika ndoa na uchumba kwa njia ya barua pepe kupitia anuani pepe ya mshauriwa.
Hapa mbele, nategemea kuwa nitakuwa natoa makala ya masuala ya afya na usimamizi wa biashara. Lakini hii itategemea zaidi na ushauri, maoni na mahitaji ya wasomaji wa Blogu hii.
Pia kwa kupitia blogu hii, tutatoa vitabu na majarida mbalimbali kwa njia mtandao na chapisho na Ili kupata makala husika utalazimika kuchangia kidogo.

CHANGAMOTO ZILIZO KATIKA NDOA NA UCHUMBA
Changamoto katika ndoa na uchumba zinaweza kugawanywa katika Makundi makuu mawili kwa mtazamo wa visababishi/vyanzo vya changamoto-
Ø  Zinazoletwa na watu wanaowazunguka.

Ø  Zinazoletwa na wao wenye.

Ø  Zinazoletwa na watu wanaowazunguka na pamoja na wao wenyewe
Changamoto zote hizo zote kila moja utatuzi wake umekuwa mgumu sana kwa sababu taasisi za kidini ambazo ndio mtatuzi mkuu wa changamoto hizi zinahitaji kusaidiwa na Blogu hii itafanya kazi hii ya usaidizi. Na pia baadhi ya masheikh na wachungaji wamekosa maadili yaani; usiri wa matatizo wanayoletewa na waumini wao. Pia marafiki na ndugu wengi wamekuwa hawana msaada, badala yake wamekuwa watoaji wakubwa wa changamoto za wanadoa na wachumba na inakuwa chanzo cha kuvunjika kwa ndoa na uchumba mwingi.
 Kwa kupitia blogu hii utapata ushauri wo wote utakaohitaji katika masuala ya ndoa na uchumba na daima itabaki siri baina yako na mshauri wa Blogu hii.
MADHARA YANAYOLETWA NA CHANGAMOTO KATIKA NDOA NA UCHUMBA
Ø  Taraka/Kuacha.

Ø  Watoto wa mitaani.

Ø  Kukata tamaa ya maisha.

Ø  Kujinyoka na kujiua kwa sumu/risasi.

Ø  Kuua watoto.

Ø  Utoaji Mimba.

Ø  Uasi wa kupitiliza .n.k.
USHAURI
Napenda kukushauri kwamba kwa kusoma makala za Blogu hii, ambazo nategemea kuwa nitakuwa nazitoa kwa juma mara moja utapata mbinu muafaka za kukabiliana na changamoto zinazoletwa na matatizo ya kimahusiano katika ndoa na uchumba.
Mnakaribishwa kuomba ushauri wa changamoto zinazowakabili katika masuala ya ndoa na uchumba kwa kupitia e_mail yangu ya fkmwamoto@gmail.com