Friday 24 April 2015

MCHAKATO WA KUPATA MCHUMBA

Habari za siku nyingi ndugu zangu wapenzi wa wavuti hii. Bila shaka kwa uwezo wa mwenyezi Mungu ni wazima na buheri wa afya.
 Leo napenda kuongelea mchakato wa kupata mchumba. Katika maisha ya hivi sana kuna changamoto nyingi sana kwa vijana hata watu wazima wanaohitaji kupata wenzi wao wa maisha. Changamoto hii, inakuja kutokana na kutokujua ni mchakato gani wapitie katika zoezi hili la kutafuta mchumba/mwenza wake wa maisha. Mchakato kwa tafsiri isiyo rasmi ni mtiririko wa matokeo ili kuweza kufikia hatua iliyokusudiwa. Mchakato wa kupata mchumba kwa watu makini ni kama ifuatavyo kwa mpangilio:-
1.       Kumuomba Mungu akupatie mchumba.
2.       Kutafuta rafike ambayo anaweza kuwa mchumba mtarajiwa
3.       Kumtafuta mchumba mtarajiwa
4.       Kupata mchumba mtarajiwa
5.       Kumshukuru Mungu kwa kukupatia mchumba
6.       Msichana/Mwanamke kuwajulisha wazazi wake kwamba amepata mchumba
7.       Mvulana/mwanaume kwenda kwa wazazi wa mwanamke kuchumbia
8.       Kuoana
Ufafanuzi wa kila hatua utafuata kwenye mwendelezo wa makala hii wiki ijayo.
Nakuomba uwaalike marafiki na nduguzo kutembelea wavuti hii, ili kupata maarifa ya masuala ya uchumba na mahusiano.

No comments:

Post a Comment