Wednesday 30 July 2014

MATARAJIO YA WANANDOA KWENYE MAISHA YA NDOA

Wanandoa huwa na matarajio mengi sana katika maisha yao ya ndoa hasa matarajio mazuri daima.  Maisha ya ndoa ni mchakato ambao hupita katika hatua kuu nne (4) yaani; kuzaliwa, kukua, kuzeeka na kufa. Lakini si ndoa zote hupitia hatua hizo zote nne (4) baadhi hupitia hatua tatu (3) au mbili (2) kutokana na baadhi ya wanandoa kuacha kumkabidhi mlezi na mwanzilishi wa ndoa duniani yaani; Mungu. Kwenye makala hii, sitaki kuongelea sababu anuai zinazosababisha baadhi ya ndoa kutopitia hatua kuu nne (4) mzunguko wa maisha ya ndoa. Baadhi ya matarajio maisha ya iliyo katika hatua ya pili (2) ni kama yafuatavyo:-
ü  Changamoto za masuala ya kifedha.
ü  Changamoto za kimawasiliano baina yao.
ü  Changamoto zinazoletwa na wanandugu na watoto.
ü  Upweke.
ü  Kukua/kudumaa kiroho.
ü  Migogoro.
ü  Magonjwa.
Kipengere cha 4 hadi 7 nitavifafanua lakini cha 1 hadi 3 zilishavifanunua kwenye makala zangu za awali za changangamoto zinazosababishwa na wanandoa wenyewe na changamoto zinazosababishwa watu wengine wasiyowanandoa.
Upweke; Kutokana na kuongezeka kwa majukumu na uwajibikaji kwa masuala ya kifamilia maisha uliyokuwa unategemea kuwa yatakuwa daima ya amani na furaha huanza kubadilika na hapo ndipo hali ya kutaka kukaa kiupweke uanza kujitokeza ili kutafari zaidi majukumu ya kifamilia na hamu ya tendo la ndoa hupungua kwa sababu ubongo unakuwa umezingirwa na mawazo ya namna ya kutatua majukumu yaliyo mbele kama vile ada, kodi ya nyumba, gharama za usafiri kwenda na kurudi kazini, chakula nakadhalika.
Migogoro; Kutokana ndoa kuwa katika hatua ya kukua  tabia zote zilizokuwa zimevichwa na wanandoa wote uanza kudhihirika kwa sababu tabia haiwezi kufichwa daima. Tabia za kiburi, jeuri, dharau, hasira, uasherati nakadhalika uanza kuonekana na kuleta migogoro ya hapo pale katika ndoa. Hatua hii inahitaji busara na hekima kubwa hasa kwa kumshirikisha Mungu, ili kuweza kuivuka na ndoa nyingi sana huishia hatua hii.
Magonjwa; Kwa sababu za kimazingira na vyakula imekuwa ni jambo la kawaida kwa binadamu kuugua kwa muda mrefu au mfupi. Inapotokea uuguaji ni wa muda mrefu jambo ili uyumbisha sana hali ya uchumi wa wanandoa na kama hakuna upendo wa dhati basi hata misingi ya ndoa uanza kulegalega.
Mwacheni Mungu awe mtawala katika maisha yenu ya ndoa kwa maana yeye ndie muasisi ya taasisi ya ndoa hakika ndoa yenu itadumu na itakuwa kisima cha amani na furaha. Na pia nakushauri ujiunga na blogu ya http://mkombozi-mahusiano.blogspot.com kwa TZS. 10,000.00 kupitia huduma ya Tigo na  Aairtel Money  kupitia  0719841988 na 0784190882 upate makala zenye maarifa tele ya masuala ya mahusiano.
Jiunge na blogu tajwa hapo UPATE MAARIFA YA KUPUNGUZA MIGOGORO KATIKA MAHUSIANO, TUJENGE TAIFA IMARA.





No comments:

Post a Comment